Vibibi
Vipimo Mchele 2 Vikombe Tui la nazi 1 1/2 Kikombe Mafuta 1 kijiko cha supu Hamira 2 Vijiko vya chai Unga wa ngano 1 kijiko cha supu Hiliki kiasi upendavyo Sukari ¾ au 1 Kikombe Namna Ya Kupika Na Kutayarisha 1· Osha na roweka mchele usiku mzima ndani ya maji baridi. 2· Mimina vifaa vyote isipokuwa sukari , ndani ya mashine ya kusagia (blender) na usage mpaka mchele uwe laini. 3· Mimina ndani ya bakuli na ufinike , kisha weka pahali penye joto ili mchanganyiko ufure. 4· Ukishafura , mimina sukari na changanya vizuri ; ukiona mchanganyiko ni mzito 5· Weka chuma kipate moto. 6· Paka mafuta au samli kidogo kwenye chuma kisha mimina mchanganyiko kiasi kuunda duara na ufunike. 7· Utazame ikishaiva upande mmoja , geuza upande wa pili mpaka iwe tayari. 8· Endelea Mpaka umalize mchanganyiko wote; panga kwenye sahani na tayari kuliwa. Kidokezo
|
- Login or register to post comments
- Email this page
- Chapisha



As-salaam Aleikum na shukran
As-salaam Aleikum na shukran nyingi
Mbali na kutumia non-stick pan , ni mbinu gani nitatumie ili vibibi visigande ikiwa ninatumia chuma
changu cha kawaida.
Maasalaam