Ladu

VIPIMO
Unga 6 vikombe
Samli ½kikombe
Baking Powder ½kijiko cha chai
Maziwa 1 kikombe
Maji Kisia kiasi
VIPIMO VYA SHIRA
Sukari
Maji
Vanilla
kungumanga
NAMNA YA KUTAYARISHA NA KUPIKA
1) Changanya unga wa dengu, samli, baking powder pamoja na maziwa katika mashine ya keki (cake mixer).
2) Ukisha changanya angalia kama mchanganyiko wako umekua mwepesi kidogo kuliko wa keki,
3) Kisha weka mafuta kiasi kwenye karai,weka na samli kikombe kimoja, weka kwenye moto wa kiasi.
5) Pika ndani ya mafuta mpaka iwive, ila usiache ikawa brown.
6) Toa mchanganyiko ulowiva tia ndani ya shira uliyo pika. Hakikisha shira iwe imepoa kabla ya kutia mchanganyiko huo.
7) Endelea kupika mchanganyiko wako mpaka uishe, kila ukitoa katika mafuta hakikisha unatia ndani ya shira.
8) ukishamaliza wote kanda huo mchanganyiko ulokua ndani ya shira mpaka uone shira yote imekauka (yaani iwe imeingia ndani ya mchanganyiko).
9) Tupia zabibu kavu na lozi zilizo katwa, changanya na mkono.
10) Wacha mchanganyiko katika bakuli, funika na foil mpaka siku ya pili.
11) Siku ya pili chukua mchanganyiko kiasi katika mkono tengeneza mviringo (round).
NAMNA YA KUTAYARISHA SHIRA
1) Katika sufuria, tia sukari, maji, kungumanga, vanilla na rangi.
2) weka kwenye moto wacha ichemke mpaka itowe povu (bubbles) juu.
3) Kisha toa povu, wacha shira kwenye moto
4) Hakikisha shira yako iwe inanata kiasi kwenye vidole, lakini iwe nyepesi kidogo kuliko shira ya kaimati.
- Login or register to post comments
- Email this page
- Chapisha


