Skip navigation.
Home kabah

Kaimati Za Shira Ya Tende

VIPIMO

Unga                                                   2 vikombe

Hamira                                               1 Kijiko cha chai

Samli imoto                                        2 Kijiko vya Supu

Maziwa au Tui la nazi                        1 ½ Kikombe cha chai (inategemea  kikombe)

Mafuta ya kukaangia                         Kiasi

Shira ya Tende   (Ya Tayari)             Kiasi

 

 

NAMNA YA KUTAYARISHA NA KUPIKA

 

1)    Pasha Samli iwe moto kabisa.

2)    Changanya unga  Hamira, Samli, Maziwa Au Tui la nazi kisha

       vuruga kama unga wa kaimati za kawaida.

3)    Ukiuumuka (ukifura) choma kaimati katika mafuta ya moto kama

       kawaida ya kuchoma kaimati.

4)    Ziepue na zichuje mafuta.

5)    Zitie katika bakuli au sahani na mwagia Shira ya Tende kiasi

       upendavyo. Tayari kuliwa.

Kidokezo: Unaweza kutumia shira ya kawaida ukipenda badala ya tende