Custard Ya Mdalasini

VIPIMO
Maziwa 2 1/2 Vikombe
Mdalasini wa unga 1 Kijiko cha chai
Mayai 3
Asali 1/4 Kikombe
Chumvi Kidogo (dash)
Vanilla 1 Kijiko cha chai
NAMNA YA KUTAYARISHA NA KUPIKA
1. Washa oveni moto wa 375F.
2. Weka vibakuli 6 maalum (remekins) vya kupikia kwenye oven , katika trei ya kuvumbika (bake).
3. Pasha moto maziwa, mdalasini na vanilla katika sufuria.
4. Chukuwa bakuli na uchanganye mayai, asali na chumvi pamoja.
5. Endelea kukoroga, huku unamimina ule mchanganyiko wa maziwa
kidogo kidogo hadi ichanganyikane vizuri.
6. Mimina huwo mchanganyiko wa custard kwenye vibakuli ulivyovitayarisha, kisha weka treya
kwenye mlango wa oveni na umimine maji ya moto (yaliyochemka) ili
itapakae chini ya vile vibakuli nusu yake.
7. Pika (bake) katika oven kwa muda wa dakika 30-40 au mpaka ukitovya kisu kitoke kisafi.
8. Ikisha iiva na kupoa, weka ndani ya friji na ikishapata ubaridi
itakuwa tayari kwa kuliwa.
- Login or register to post comments
- Chapisha
- Kutuma Kwa Email

samahani katika vipimo
samahani katika vipimo hakuna hiyo custard au unamaana mchanganyiko ndio custard?
mashallah vyakula vyote
mashallah vyakula vyote vizuri. custard ya unga wake wenyewe unaitengeneza vp?
Assalaamu 'alaykum Samahani
Assalaamu 'alaykum
Samahani nimetambua kuwa vipimo vimeleta utata kidogo, ni kweli hakuna custard kwenye orodha ya vipimo! huwo mchanganyiko ndio custard yenyewe. Insha Allah tumefahamiana.