Skip navigation.
Home kabah

Custard Ya Mdalasini



VIPIMO


Maziwa                                                 2 1/2 Vikombe

Mdalasini wa unga                               1 Kijiko cha chai

                           
Mayai                                                   3


Asali                                                     1/4 Kikombe

 

Chumvi                                                 Kidogo (dash)


Vanilla                                                  1 Kijiko cha chai


NAMNA YA KUTAYARISHA NA KUPIKA


1.         Washa oveni moto wa 375F.


2.         Weka vibakuli 6 maalum (remekins) vya kupikia kwenye oven , katika trei ya                        kuvumbika (bake).


3.         Pasha moto maziwa, mdalasini na vanilla katika sufuria.


4.         Chukuwa bakuli na uchanganye mayai, asali na chumvi pamoja.


5.         Endelea kukoroga, huku unamimina ule mchanganyiko wa maziwa

            kidogo kidogo hadi ichanganyikane vizuri.


6.         Mimina custard kwenye vibakuli ulivyovitayarisha, kisha weka treya

            kwenye mlango wa oveni na umimine maji ya moto (yaliyochemka) ili

            itapakae chini ya vile vibakuli nusu yake.


7.         Pika (bake) katika oven kwa muda wa dakika 30-40 au mpaka ukitovya                     kisu kitoke kisafi.


8.         Ikisha iiva na kupoa, weka ndani ya friji na ikishapata ubaridi

             itakuwa tayari kwa kuliwa.