Kastadi Ya Tambi

Vipimo
Tambi nyembamba za hudhurungi (brown) 1/2 pakiti
Maziwa mazito (condensed milk) 1/2 kikopo
Maziwa ya kawaida 5 kiasi ya vikombe
Sukari 1/4 kikombe
Kastadi 2 vijiko vya supu
Hiliki 1/4 kijiko cha chai
Kungumanga 1/2 kijiko cha chai
Zaafarani(roweka katika 1/4 kikombe maji) 1 kijiko cha chai
Vanilla 1 kijiko cha chai
Lozi za kukata au njugu za pistachio 1/2 kikombe
Namna Ya Kutayarisha Na Kupika:
1. Katakata tambi kabisa.
2. Katika sufuria tia maziwa kisha uchanganye na kastadi ukoroge.
3. Eka katika moto, tia maziwa mazito (condensed milk), sukari hiliki, kungumanga, zaafarani na vanilla iache ichemke huku unakoroga bila ya kuachia mkoni ili isifanye madonge.
4. Ukiona imekuwa nzito ongeza maziwa mepesi iwe
5. Tia tambi uendelee kukoroga usiache mkono, ziache kidogo tu ziive epua na umimine katika bakuli iache ipowe.
6. Mwagia lozi juu yake.
7. Tia kwenye friji ikiwa baridi iko tayari.
- Login or register to post comments
- Email this page
- Chapisha
