48-Dalili Za Kheri Katika Mambo Yamfaayo Maiti: Kumlipia maiti saumu

 

Kumlipia maiti saumu:

 

Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa Sallam) amesema, “ Atakayekufa ilhali kaacha deni la funga basi na alipiwe na walii wake.” (Bukhari na Muslim)

Katika sahihi mbili tunasoma: kuwa mwanamke fulani alisafiri baharini akapanda chombo akanadhiria kwa Mwenyezi Mungu kuwa akimuokoa atafunga mwezi mzima, Mwenyezi Mungu akamuokoa lakini hakufunga hadi alipofariki. Wakaja jamaa zake wa karibu kama sio dada yake basi alikuwa ni bintie akaenda kwa Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa Sallam) akamueleza kuhusu ile nadhiri ya funga ya mama yake. Mtume akamuuliza, “Je, unaonaje je, angelikuwa anadaiwa na mtu si ungemlipia deni lile?” yule binti akajibu, ‘Ndio’ kisha Mtume akamwambia, “basi mlipie funga yake.” Hali kadhalika linaingia hapo funga zote za wajibu na za kunadhiria.

Share