Kufuata Rai Katika Mas-ala Ya Dini
SWALI:
Ndugu zangu na Masheikh zangu,
Assalaam alaykum,
Katika kujibu swali linalohusu "Mas-hul-khufayyn" Mlijibu kama kuna tafauti ya RAI miongoni mwa Maulamaa.
Katika kuendelea kujibu swali
Naomba ufafanuzi zaidi kuhusu masaala haya ya kufuata RAI.
Natumai nimefahamika.
Ahsanteni
JIBU:
Sifa zote njema Anastahiki Allaah Aliyetukuka Mola Mlezi wa walimwengu wote, Swalah na salamu zimshukie kipenzi chetu Mtume Muhammad (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) na Swahaba zake (Radhiya Allaahu ‘anhum) na watangu wema mpaka Siku ya Mwisho
Tunashukuru kwa mchango wako mzuri.
Tunapenda kufafanua
((وَمَا كَانَ لِمُؤْمِنٍ وَلَا مُؤْمِنَةٍ إِذَا قَضَى اللَّهُ وَرَسُولُهُ أَمْرًا أَن يَكُونَ لَهُمُ الْخِيَرَةُ مِنْ أَمْرِهِمْ وَمَن يَعْصِ اللَّهَ وَرَسُولَهُ فَقَدْ ضَلَّ ضَلَالًا مُّبِينًا))
((Haiwi kwa Muumini mwanamume wala Muumini mwanamke kuwa na khiari katika jambo, Allaah na Mtume Wake Wanapokata shauri katika jambo lao. Na mwenye kumuasi Allaah na Mtume Wake basi hakika amepotea upotofu ulio wazi)) [Al-Ahzaab: 36]
Na ndipo ukaona maneno ya 'Aliy (Radhiya Allaahu 'anhu) aliposema kuwa hii dini haiendi kwa rai kwa maana kuwa Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alishaamua wapi pa kupanguswa soksi za ngozi (khuff)
"لو كان الدين بالرأي لكان أسفل الخف أولى بالمسح من أعلاه , لقد رأيت رسول الله صلى الله عليه وسلم يمسح على ظاهر خفيه" رواه أبو داود والدارقطني .
Ingelikuwa dini inakwenda kwa rai ingelikuwa kupangusa chini ya khuff (soksi za ngozi) ni bora zaidi kuliko juu. Hakika nimemuona Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa alihi wa sallam) anapangusa juu ya khuff (soksi za ngozi)” [Imepokelwa na Abu Daawuud na ad-Daaraqutwniy]
Japokuwa inaweza isiingie kwenye akili za hao wenye kutumia rai tu na kutegemea rai kwa kila kitu na kila sehemu na wakaona kwa nini kusipanguswe chini penye kukanyagiwa ambapo ndipo panapokusanya uchafu? Na akamalizia 'Aliy (Radhiya Allaahu 'anhu) kwa kusema kuwa hivyo ndivyo alivyofanya Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) kwa maana hata
Ama rai katika Dini inakubalika pale ambapo hakuna dalili iliyo wazi katika masuala fulani. Na kwa upande mwengine hujulikana hizo rai kama ni Ijtihaad na pia
عَنْ مُعَاذٍ أَنَّ رَسُولَ اللهِ صلى الله عليه وسلم حِينَ بَعَثَهُ إِلَى الْيَمَنِ ، فَقَالَ (( كَيْفَ تَصْنَعُ إِنْ عَرَضَ لَكَ قَضَاءٌ؟)) قَالَ : أَقْضِي بِمَا فِي كِتَابِ اللهِ ، قَالَ (( فَإِنْ لَمْ يَكُنْ فِي كِتَابِ اللهِ؟)) قَالَ : فَسُنَّةُ رَسُولِ الله ، قَالَ : ((فَإِنْ لَمْ يَكُنْ فِي سُنَّةِ رَسُولِ الله؟)) قَالَ : أَجْتَهِدُ رَأْيِي لاَ آلُو ، قَالَ : فَضَرَبَ رَسُولُ اللهِ صلى الله عليه وسلم صَدْرِي ، ثُمَّ قَالَ : ((الْحَمْدُ ِللهِ الَّذِي وَفَّقَ رَسُولَ رَسُولِ اللهِ لِمَا يُرْضِي رَسُولَ الله)) سنن أبي داود
Kutoka kwa Mu’aadh kwamba Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa alihi wa sallam) alipomtuma
Hadiyth hii kama tulivyoeleza juu, ni kuwa wamekhitalifiana
Ingawa kisa hichi pamoja na utata wake wa usahihi lakini kinaungwa mkono na kauli za Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala) zifuatazo katika mas-ala haya ya kufuata wale Uwlul-Amr:
((يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُواْ أَطِيعُواْ اللّهَ وَأَطِيعُواْ الرَّسُولَ وَأُوْلِي الأَمْرِ مِنكُمْ فَإِن تَنَازَعْتُمْ فِي شَيْءٍ فَرُدُّوهُ إِلَى اللّهِ وَالرَّسُولِ إِن كُنتُمْ تُؤْمِنُونَ بِاللّهِ وَالْيَوْمِ الآخِرِ ذَلِكَ خَيْرٌ وَأَحْسَنُ تَأْوِيلاً))
Enyi mlioamini! Mtiini Mwenyezi Mungu, na mtiini Mtume na wenye madaraka katika nyinyi. Na mkizozana katika jambo basi lirudisheni kwa Mwenyezi Mungu na Mtume, ikiwa mnamuamini Mwenyezi Mungu na Siku ya Mwisho. Hayo ndiyo bora zaidi na ndiyo yenye mwisho mwema)) [An-Nisaa: 59]
((وَإِذَا جَاءهُمْ أَمْرٌ مِّنَ الأَمْنِ أَوِ الْخَوْفِ أَذَاعُواْ بِهِ وَلَوْ رَدُّوهُ إِلَى الرَّسُولِ وَإِلَى أُوْلِي الأَمْرِ مِنْهُمْ لَعَلِمَهُ الَّذِينَ يَسْتَنبِطُونَهُ مِنْهُمْ))
((Na linapowafikia jambo lolote la amani au la khofu hulitangaza. Na kama wangalipelilipelekea kwa Mtume na kwa wenye mamala kwao, wale wanaopeleleza (anaojua
Hivyo masuala ya rai yanakubalika pale ambapo hiyo rai haitapingana au kugongana na Qur-aan au Sunnah sahihi. Na ndio maana ukaona kuna madhehebu hizi nne na wakawa wanatofautiana katika mas-ala mbalimbali ya ki-Fiqhi. Na ma-Imaam wote wa madhehebu hizo wakawa wanaheshimiwa kwa elimu zao na Ijtihaad zao, kwa kuwa vilevile Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) keshaeleza kuwa atakayejitahidi (Kiongozi, Imaam, 'Aalim, Mujtahid) na akapata basi ana ujira mbili na atakayekosa ana ujira mmoja (al-Bukhaariy na Muslim).
Yote hayo ni katika kuonyesha rai ambayo inawafikiana au kutopingana na Qur-aan na Sunnah sahihi basi inakubalika katika Dini.
Wa Allaahu A'alam
- Login or register to post comments
- Email this page
- Chapisha


