Skip navigation.
Home kabah

Je, Utapokea Kitabu Chako Kwa Mkono Gani?

 

10 Muharram 1429 

Anasema Allaah سبحانه وتعالى  

(( وَوُضِعَ الْكِتَابُ فَتَرَى الْمُجْرِمِينَ مُشْفِقِينَ مِمَّا فِيهِ وَيَقُولُونَ يَا وَيْلَتَنَا مَالِ هَذَا الْكِتَابِ لَا يُغَادِرُ صَغِيرَةً وَلاَ كَبِيرَةً إِلاَّ أَحْصَاهَا وَوَجَدُوا مَا عَمِلُوا حَاضِرًا وَلاَ يَظْلِمُ رَبُّكَ أَحَدًا))

Na kitawekwa kitabu. Basi utawaona wakosefu wanavyoogopa kwa yale yaliomo humo. Na watasema: Ole wetu! Kitabu hichi kina nini! Hakiachi dogo wala kubwa ila huliandika? Na watayakuta yote waliyoyatenda yamehudhuria hapo. Na Mola wako Mlezi Hamdhulumu yeyote(( [Al-Kahf:49]

Aayah hii ni kama kawaida ya aya za Qur-aan, huwa zinampa mtu picha fulani ya yale masimulio yanayosimuliwa, na Aayah hii inatupa picha ya  baadhi ya matukio makubwa yatakayotokea siku ya Qiyaamah. Siku isiyo na shaka, siku ya miadi, siku ya inayosubiriwa,  siku ya majuto, siku ya nyoyo kushituka na macho kukodoka, siku ya mashaka, siku ambayo hakuna budi kwa kila mmoja kukutana nayo. 

Naam ndugu Waislamu hii ni siku ya Hisaab kulipwa mema au mabaya, Siku wanayonyanyuka watu wote na majini kwa Mola wa Ulimwengu, siku ambayo:

 ((وَيَقُولُ الْكَافِرُ يَا لَيْتَنِي كُنتُ تُرَابًا))

 ((na kafiri atasema: Laiti ningeli kuwa udongo!)) [An-Nabaa:40]

Je, Umefikiria na kuwaza ndugu Muislamu hali yako itakavyokuwa siku hiyo utakaposimama mbele ya Mola wako Mtukufu na huku unasubiri hesabu upewe kitabu chako? Mmoja wetu anapoingia kufanya mtihani au anapokwenda mahakamani kuhukumiwa, moyo wake huwa unadunda hadi unakaribia kutoka katika kifua kwa khofu ya kutaka kujua atafanyaje au yapi yatakuwa matokeo yake. Je, itakuwaje hali ya moyo siku hiyo wakati matokeo yake yatakuwa ni aidha Pepo ya milele yenye maisha ya raha au moto wenye adhabu kali?  Khaswa ikiwa umeishi umri wako wote katika maasi au umezama katika starehe ya dunia bila kuchuma mema yoyote, vipi itakuwa hali yako siku hiyo?  Subhana Allaah!

Jihesabu leo kabla ya kesho ndugu Muislamu, tutazame maneno mazito ya hekima kutoka kwa Amiyrul Muuminiyn:

 يقول عمر بن الخطاب رضي الله عنه: "حاسبوا أنفسكم قبل أن تحاسبوا، وزنوها قبل أن توزنوا، فإن أهون عليكم في الحساب غدًا أن تحاسبوا أنفسكم اليوم، وتزينوا للعرض الأكبر،  ((يومئذ تعرضون لا تخفى منكم خافية))      

 Anasema 'Umar Ibn Al-Khatwaab رضي الله عنه "Hesabuni nafsi zenu kabla ya kuhesabiwa, na zipimeni kabla ya kupimwa, kwani ni bora (wepesi)  kwenu kupima (amali zenu) leo kabla ya (kupimwa) kesho kwenye Hesaabu, na jipambieni kwa siku ya Hadhara kuu, ((Siku hiyo mtahudhuriwshwa haitafichika siri yoyote))" [Al-Haaqah:18]  

Jipime ndugu Muislamu na jiulize, Je, utakuwa miongoni mwa watakaopewa vitabu vyao mkono wa kulia ukakichukua kwa furaha kubwa na kukionyesha kwa wenzako kama unapopata shahada yako ambayo umefuzu vizuri sana na ukatamani kila mmoja aione! Na uwaambie kwa furaha 'Nimefuzu! Nimefuzu vizuri sana! Kama Anavyosema Allaah: 

 ((فَأَمَّا مَنْ أُوتِيَ كِتَابَهُ بِيَمِينِهِ فَيَقُولُ هَاؤُمُ اقْرَؤُوا كِتَابِيهْ)) ((إِنِّي ظَنَنتُ أَنِّي مُلَاقٍ حِسَابِيهْ))  ((فَهُوَ فِي عِيشَةٍ رَّاضِيَةٍ))  ((فِي جَنَّةٍ عَالِيَةٍ))  ((قُطُوفُهَا دَانِيَةٌ))    ((كُلُوا وَاشْرَبُوا هَنِيئًا بِمَا أَسْلَفْتُمْ فِي الأََيَّامِ الْخَالِيَة))

 ((Basi ama atakayepewa kitabu chake kwa mkono wake wa kulia, atasema: Haya someni kitabu changu!)) ((Hakika nalijua ya kuwa nitapokea hisabu yangu)) ((Basi yeye atakuwa katika maisha ya kupendeza)) ((Katika Bustani ya juu)) ((Matunda yake yakaribu)) ((Waambiwe: Kuleni na mnywe kwa furaha kwa sababu ya mlivyo tanguliza katika siku zilizo pita)) [Al-Haaqah: 19-24]

Au utakuwa miongoni mwa wale watakaopewa katika mkono wa kushoto ukawa na majuto makubwa usiyoyaweza kuyarekebisha tena? Kama Asemavyo Allaah:

(( وَأَمَّا مَنْ أُوتِيَ كِتَابَهُ بِشِمَالِهِ فَيَقُولُ يَا لَيْتَنِي لَمْ أُوتَ كِتَابِيهْ)) ((وَلَمْ أَدْرِ مَا حِسَابِيهْ))  

((Na ama atakayepewa kitabu chake katika mkono wake wa kushoto, basi yeye atasema: Laiti nisingelipewa kitabu changu!)) ((Wala nisingelijua nini hisabu yangu))

Majuto yanazidi kuwa makubwa hadi ukayatamani mauti kuliko haya!

((يَا لَيْتَهَا كَانَتِ الْقَاضِيَةَ)) ((مَا أَغْنَى عَنِّي مَالِيهْ))   ((هَلَكَ عَنِّي سُلْطَانِيهْ))

((Laiti mauti ndiyo yangelikuwa ya kunimaliza kabisa)) ((Mali yangu hayakunifaa kitu)) ((Madaraka yangu yamenipotea))

Wataamrishwa Malaika wakuchukue na wakutupe motoni!  Ikiwa Malaika mmoja tu hutoweza kushindana naye kwa nguvu zake ndugu Muislamu, itakuwaje kundi la Malaika?

  ((خُذُوهُ فَغُلُّوهُ)) ((ثُمَّ الْجَحِيمَ صَلُّوهُ)) ((ثُمَّ فِي سِلْسِلَةٍ ذَرْعُهَا سَبْعُونَ ذِرَاعًا فَاسْلُكُوهُ))

(([Pasemwe]: Mshikeni! Mtieni pingu!)) ((Kisha mtupeni Motoni!)) ((Tena mtatizeni katika mnyororo wenye urefu wa dhiraa sabiini!))

Kwa nini uwe katika hali hiyo? Na'am, ni kwa kuwa...

  ((إِنَّهُ كَانَ لاَ يُؤْمِنُ بِاللَّهِ الْعَظِيمِ))

((Kwani huyo hakika alikuwa hamuamini Mwenyezi Mungu Mtukufu))

Hukuamini amri Zake na makatazo Yake pamoja na aliyokuja nayo Mtume صلى الله عليه وآله وسلم .  Wala …

   ((وَلاَ يَحُضُّ عَلَى طَعَامِ الْمِسْكِينِ))

((Wala hahimizi kulisha masikini))

Na kama sababu ilikuwa umeshughulika na ndugu au jamaa au  rafiki zako, basi leo hakuna hata mmoja atakeyekufaa, kila mmoja atakuwa analo lake la kukhofia...

  (( فَلَيْسَ لَهُ الْيَوْمَ هَاهُنَا حَمِيمٌ))

((Basi leo hapa hana jamaa wa kumwonea uchungu))

Na chakula kibaya mno humo motoni kama usaha unaotoka katika miili ya watu na mti wa Zakkuum ambao mchungu ajabu na una miba, mti unaotisha kabisa!

 ((وَلاَ طَعَامٌ إِلاَّ مِنْ غِسْلِينٍ))  (( لاَ يَأْكُلُهُ إِلاَّ الْخَاطِؤُونَ))  

((Wala hana chakula ila usaha wa watu wa Motoni)) ((Chakula hicho hawakili ila wakosefu))

[Al-Haaqah: 25-37 ]

Umeridhika ndugu Muislamu uwe katika hali hiyo mbaya? Umeridhika kuwa umeacha kuswali, kufunga, na kufanya mema? Umeridhika kupoteza wakati wako kwa mambo ya upuuzi? Umeridhika kumuasi Mola wako Mtukufu Atakayekusimamisha ujibu kila baya ulilolifanya pale utakapokuta kitabu chako ambacho hakikuacha kubwa wala dogo?

Anasema Allaah سبحانه وتعالى katika Hadiythil-Qudsiyy

((ياعبادي إنما هي أعمالكم  أحصيها لكم فمن وجد خيراً فليحمد الله ومن وجد غير ذلك فلا يلومن إلا نفسه)) مسلم

((Enyi waja Wangu, ni vitendo vyenu Ninavyovihesabu, kwa ajili yenu Nikakulipeni.  Kwa hivyo anayekuta wema amshukuru Allaah na yule anayekuta yasiokuwa mema (basi) ajilaumu mwenyewe)) [Muslim]

Allaahumma tujaaliye tuwe miongoni mwa wale watakaopewa vitabu vyao mkono wa kulia.   Aamiyn

((فَأَمَّا مَنْ أُوتِيَ كِتَابَهُ بِيَمِينِهِ))   ((فَسَوْفَ يُحَاسَبُ حِسَابًا يَسِيرًا )) ((وَيَنقَلِبُ إِلَى أَهْلِهِ مَسْرُورًا))

(( Ama atakayepewa daftari lake kwa mkono wa kulia)) ((Basi huyo atahisabiwa hisabu nyepesi)) ((Na arudi kwa ahli zake na furaha)) [Al-Inshiqaaq: 7-9]

Na usitujaalie tukawa miongoni mwa wale watakaopewa vitabu vyao katika mkono wa kushoto au nyuma ya migongo yao:

 ((وَأَمَّا مَنْ أُوتِيَ كِتَابَهُ وَرَاء ظَهْرِهِ))  ((فَسَوْفَ يَدْعُو ثُبُورًا ))    ((وَيَصْلَى سَعِيرًا)) 

((Na ama atakayepewa daftari lake kwa nyuma ya mgongo wake)) ((Basi huyo ataomba kuteketea)) ((Na ataingia Motoni))  [Al-Inshiqaaq: 10-12]

 

******************