Masuala Kumi Yanayoeleweka Vibaya Katika Uislam - 7
Chuo Kikuu Cha California Ya Kusini
USC-MSA Muhtasari Ya Maandiko Ya Waislamu
Imefasiriwa na: ‘Abdun-Naaswir Hikmany
Suala Nambari 7 Linaloeleweka Vibaya
Uislamu unakubali kuwaua watu wasio na hatia kwa sababu:
· Waislamu wanaweza kuwa ni magaidi
· Waislamu wanashiriki kwenye ‘vita tukufu’ (jihaad)
· Uislamu umeenea kwa panga
· Ni mfumo wa kisheria ulio katili na dhalimu
Siku hizi, suala hili linaloeleweka vibaya ni miongoni mwa lililoenezwa mno kabisa kuhusu Uislamu. Lakini bado ndani ya Qur-aan, Muumba Anaeleza bila ya utata (tafsiri):
{{Wala msiue nafsi ambayo Mwenyezi Mungu amekataza (kuiua) isipokuwa kwa haki (Akahuhumu hakimu kuwa mtu huyo anastahiki kuuawa na akatoa amri ya kuuawa). Na mwenye kuuawa kwa kudhulumiwa, basi Tumempa nguvu mrithi wake (juu ya muuaji huyo, akitaka ataomba kwa hakimu kuwa amuuwe
Tukiegemea kwenye aya hii, hairuhusiki kwa Uislamu kuua mtu yeyote asiye na kosa kwa baadhi ya makosa ya jinai. Ni vyema tukakumbuka katika nukta hii, tofauti iliyofanywa hapo juu baina ya Qur-aan na Sunnah, na Waislamu; ni Qur-aan na Sunnah pekee ndizo zilizoafikiwa kuwa zinaendana pamoja na matakwa ya Muumba, wakati Waislamu wanaweza
Na itambulike wazi basi, kwamba “Gaidi Muislamu” inafanana na maneno mawili yenye kupewa maana tofauti ili kutoa msemo mmoja oxymoron: kwa kuua watu wasio na hatia, Muislamu anatenda dhambi kubwa, na Allaah ni anayefanywa kuwa Muadilifu personified. Msemo huu ni wa kukosa nidhamu na kuushushia hadhi Uislamu, na ni lazima uepukwe. Inategemewa kwamba; kwa vile uelewa na hamasa ya Uislamu inapanda juu kwa jamii iliyo ya kawaida ya watu, basi watu watayatenganisha mbali mbali maneno ya “ugaidi” na “Uislamu”, yasitumike ndani ya msemo mmoja.
Sababu nyengine inayokuzwa ili kukubaliana na suala
{{Wameruhusiwa (kupigana) wale wanaopigwa, kwa sababu wamedhulumiwa. Na kwa yakini Mwenyezi Mungu ni Muweza wa kuwasaidia}} [22:39]
Aya hii inaweka bayana masharti kabla ya kupigana vita vyovyote ndani ya Uislamu; ni lazima kuwepo masharti ya kuwepo unyanyasaji kwa watu. Muumba Ameweka wazi amri juu yetu ya kupigana dhidi ya unyanyasaji na udhalimu, hata kama ikiwa kwa gharama ya kumwaga damu
{{Na piganeni katika njia ya Mwenyezi Mungu na wale wanaokupigeni, wala msipundikie mipaka (mkawapiga wasiokupigeni). Kwani Mwenyezi Mungu hawapendi warukao mipaka. Na waueni (hao wanaokupigeni bure) popote muwakutapo, na muwatowe popote walipokutoweni; kwani kuwaharibu watu na dini
Imesimuliwa na ‘AbduLlaah: Wakati wa kipindi fulani cha vita Ghazawat enzi za Mtume, mwanamke alikutikana ameuawa. Mtume wa Allaah hakukubaliana na kuuawa kwa wanawake na watoto.
Suala (jengine) linaloeleweka vibaya ambalo linahusiana na jihaad, kawaida linatangazwa na Waislamu wanaosema kwamba “Jihaad ni kwa kuhami mipaka.” Qur-aan na Sunnah inakataa kabisa dhana hii.
Imesimuliwa na Abuu Mussa: Mtu mmoja alikuja kwa Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) na kuuliza, “Mtu anapigana vita kwa ngawira; mwengine anapigana kwa umaarufu na wa tatu anapigana kwa kujionesha, ni yupi miongoni mwao anayepigana kwa ajili ya Allaah?” Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akasema, “Yule anayepigana kwa Neno la Allaah (yaani Uislamu) atakuwa bora, anayepigana kwa ajili ya Allaah.” [4:52:65]
Hivyo, Muumba Anatuwajibisha kupigana vita wakati wowote pale watu wanapokandamizwa vibaya hata kukosa uhuru wa kumsikiliza au kumfanyia kazi Mjumbe wa Allaah kama ilivyo ndani ya Qur-aan na Sunnah. Sayyid Qutb, mwanazuoni Muislamu maarufu anajadili kwa ufasaha dhana ya jihaad na kujihami ndani ya kitabu chake cha Mwendo wa Maili Milestones:
“
Sababu ya tatu ambayo kawaida huwa inanukuliwa kuhusu suala hili linaloeleweka vibaya katika Uislamu inasema kwamba njia hii ya maisha inakubaliana na kuuwa watu wasio na hatia kwasababu mfumo wake wa sheria ya Uislamu ni wenye ukatili usio na maana. Hoja hii ni nyepesi kwa namna mbili.
Qur-aan na Sunnah imeweka wazi kwamba sheria ya kisasi, ni juu yetu kwa mauaji na jeraha la mwili, lakini msamaha ni bora
{{Enyi mlioamini! Mmepewa ruhusa kulipa kisasi katika waliouawa – muungwana kwa muungwana, na mtumwa kwa mtumwa, na mwanamke kwa mwanamke. Na anayesamehewa na ndugu yake (yaani yule aliyeuliwa wake) basi ashikwe kulipa kwa wema, na yeye alipe (na kulipishwa) kwa ihsani. Hiyo ni tahfifu itokayo kwa Mola wenu na ni rehema. Na atakayeruka mipaka baada ya haya, basi yeye atapata adhabu iumizayo.}} [2:178]
{{Na malipo ya ubaya ni ubaya ulio sawa na (ubaya) huo; lakini anayesamehe na kusuluhisha ugomvi; ujira wake uko kwa Mwenyezi Mungu; bila shaka Yeye hawapendi madhalimu. Na wale wanaolipiza kisasi baada ya kudhulumiwa, hao hakuna njia ya kulaumiwa.
Muumba Ameamrisha sheria ya kisasi juu yetu Akitambuwa vilivyo kwamba tunaweza kuijadili. Ndani ya jamii nyingi za leo zisizokuwa za Waislamu, kuna majadiliano yanayoendelea kuhusu adhabu ya kifo. Kwa Uislamu, mjadala huu ni butu, Muumba Amekwishalitolea maamuzi suala
{{Mtakuwa nao uhai (mzuri) katika kulipiza kisasi enyi wenye akili, ili msalimike.}} [2:179]
Watu wengi pia hawapo na uelewa wa sharti zilizo kali ambazo ni lazima zitimizwe kwa sheria ya kisasi kufanyiwa kazi. Sunnah imejaa mifano ya Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) ikituonesha pale sharti za sheria ya kisasi zinapotimizwa kabla ya kufanyiwa kazi. Kwa mfano, mwizi atawajibika tu kukosa mkono wake kama bidhaa aliyoiba imevuka kiwango fulani, na
Mwisho, hoja nyengine inayokuzwa kwa suala hili linaloeleweka vibaya mno ni kwamba Uislamu ‘umeenea kwa panga’. Ni lazima ieleweke kwa sasa kwamba ni lazima daima tutofautishe baina ya Qur-aan na Sunnah na Waislamu pale inapofika hatua ya kutambua nini Muumba Ametuhitajia (sisi kufanya). Allaah Ameeleza wazi ndani ya Qur-aan (tafsiri),
{{Hakuna kulazimishwa (mtu kuingia) katika dini. Uongofu umekwisha pambanuka na upotofu. Basi anayemkataa shetani na akamwamini Mwenyezi Mungu, bila shaka yeye ameshika kishiko chenye nguvu kisichokuwa na kuvunjika. Na Mwenyezi Mungu ni Mwenye kusikia (na) Mwenye kujua.}} [2:256]
Hivyo, HAIWEZEKANI kukubali Uislamu kwa nguvu. Hata kama Waislamu wasio na uongofu watajaribu ‘kulazimisha’ Uislamu namna fulani kwa wengine, haitokubaliwa na Muumba kwa mujibu wa aya hii.
Mijadala ya taariykh ambayo inajaribu kufafanua kwamba Waislamu ‘hawajawabadili wengine kwa nguvu’ hakika ni hoja ndogo kwa mjadala uliopo hapo juu. Hata hivyo, ni vyema kubainisha kwamba (kwa mujibu wa) taariykh, Uislamu umeenea kwa njia za amani. Ujumbe wa Muumba ulifikishwa Afrika na kusini mwa mashariki ya Asia kwa wafanyabiashara walio Waislamu, na leo nchi kubwa kabisa yenye Waislamu duniani ni
Kwa mara nyengine, ni muhimu kukumbuka kwamba Allaah Anatamka kwamba HAIWEZEKANI Uislamu kulazimishwa kwa mtu, hivyo Waislamu hawaoni haja ya kujaribu!
- Login or register to post comments
- Email this page
- Chapisha


