Baba Amefariki Ameacha Mjane, Ndugu, Watoto Na Anamiliki Nyumba
SW
Asalaam aleykum, mzee amefariki kaacha nyumba 1, ndugu wa kike 2, wa kiume 1, watoto wa kike 2 na mjane 1, nyumba itagawanywaje?
JIBU:
Sifa zote njema Anastahiki Allaah Aliyetukuka Mola Mlezi wa walimwengu wote, Swalah na salamu zimshukie kipenzi chetu Mtume Muhammad (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) na Swahaba zake (Radhiya Allaahu 'anhum) na watangu wema mpaka Siku ya Mwisho.
Shukran zetu za dhati kwa swali lako kuhusu mirathi. Awali ya yote ni kuwa lazima mwanzo ikiwa mzee ana madeni basi alipiwe na ikiwa aliacha wasiya basi pia utekelezwe lakini kiwango cha kutolewa kisizidi thuluthi (1/3).
Kwa hakika, inakuwa shida kuigawa nyumba kwa warithi hivyo wanaweza kuitia thamani hiyo nyumba kisha wakagawa kulingana na kiwango cha kila mmoja. Ikiwa si hivyo basi inatakiwa igawanywe vyumba na jambo
Ama mjane kiwango chake kinafahamika vilivyo nacho ni thumuni
“Na wake zenu watapata robo mlichokiacha, ikiwa hamna mtoto. Mkiwa mna mtoto basi sehemu
Ndugu wa kiume na wa kike marehemu watarithi pia kwa kuwa marehemu hakuacha mtoto wa kiume. Kwa hiyo, binti 2 wa marehemu watapata kila mmoja thuluthi.
Jadwali ya wirathi itakuwa
|
Namba |
Uhusiano na Marehemu |
Kiwango |
Asilimia |
|
1 |
Mjane |
Thumuni (1/8) |
12.5 |
|
2 |
Binti 1 |
Thuluthi (1/3) |
33.33 |
|
3 |
Binti 2 |
Thuluthi (1/3) |
33.33 |
|
4 |
Kaka |
|
10.42 |
|
5 |
Dada 1 |
|
5.21 |
|
6 |
Dada 2 |
|
5.21 |
|
|
Jumla |
|
100.00 |
Na Allaah Anajua zaidi
- Login or register to post comments
- Email this page
- Chapisha


