Mishkaki Ya Nyama

Mishkaki Ya Nyama

Vipimo: 

Nyama steki - 4 Ratili  (2 Kilo)

Mafuta - 3 Vijiko vya supu 

Masala Ya Kuroweka Katika Nyama:  

Kitunguu saumu/thomu na tangawizi iliyosagwa - 2 kijiko cha supu

Pilipili mbichi iliyosagwa - 1 kijiko cha supu

Papai bichi kiasi lililochunwa - ½  papai

Siki nyeupe - 3 vijiko vya supu

Chumvi - kiasi

Jiyrah (cummin powder/bizari ya pilau) - 1 kijiko cha supu

Dania (coriander powder/gilgilani) - 1 kijiko cha chai

Pilipili nyekundu ya unga - 1 kijiko cha supu

Mdalasini wa unga - 1 kijiko cha chai  

Namna Ya Kutayarisha Na Kupika: 

  1. Kata nyama vipande vikubwa kubwa kiasi .
  2. Changanya masala na vitu vyote katika nyama uroweke kwa muda wa masaa mawili.  
  3. Tunga vipande vya nyama katika vijiti vya kuchomea kababu (kabaab skewers).
  4. Choma katika jiko la makaa au katika la B.B.Q kwa moto wa kiasi ukiwa unazigeuza geuza hadi nyama iwive.
  5. Epua, weka katika sahani ikiwa tayari kuliwa.

Kidokezo: 

  • Nzuri kuliwa na Hummus na mkate ya kiarabu (pita pan bread) – tazama pishi ya Hummus katika Saladi Na Sosi

 

 

 

 

Share