Shurba Ya Nyama Mbuzi Ya Ngano Za Kukobolewa Na Ya Kotimiri

Shurba Ya Nyama Mbuzi Ya Ngano Za Kukobolewa Na Ya Kotimiri

 

 

Vipimo

 

Nyama ya mbuzi – kilo 1

Ngano zilokobolewa (Quacker oats) – kikombe 1 cha chai

Kitunguu maji kilosagwa - 3

Nyanya ilosagwa – 1

Kitunguu thomu kilosagwa – vijiko 2 vya supu

Tangawizi ilosagwa –  vijiko 2 vya supu

Mdalasini – kijiti  1

Pilipili manga - kijiko 1 cha chai

Jira/uzile (cummin powder) – vijiko 2 vya chai

Gilgilani/Dania  (coriander)

Kotmiri – msongo 1  

Ndimu – vijiko 2 vya supu

 

Namna Ya Kutayarisha Na Kupika

 

  1. Weka nyama katika sufuria ya kupikia. Tia thomu, tangawizi, chumvi, bizari zote.
  2. Tia maji kiasi uchemshe nyama hadi iwive kiasi dakika 45
  3. Tia kitunguu, nyanya endelea ichemke viwive
  4. Changanya ngano katika maji kidogo kwenye kibakuli, kisha mimina katika shurba uendelee kupika kidogo tu kiasi dakika 10
  5. Tia kotimiri uliokatakata, koroga uchanganye
  6. Tia ndimu ikiwa tayari kuliwa
  7. Unapopakuwa katika kibakuli, nyunyizia kotimiri

  

Bis-swihhah wal-hanaa (kula kwa siha na kuburudika)

 

 

Share