Je, Inapasa Kufanya Ghuslu Baada Ya Kutokwa Na Manii Bila Ya Kujimai?
SWALI:
Asalam alaykum
Naomba kuuliza ikiwa mtu na mkewe wanaongea kwa njia ya simu na katika maongezi
maji wanatakiwa wakoge janaba au wakoge kikawaida tu?
Ahsante
JIBU:
BismiLLaah wa AlhamduliLLaah was-Swalaatu wa Salaamu ‘alaa Muhammad wa ‘alaa aalihi wa Aswhaabihil Kiraam, wa ba’ad:
Hakuna vibaya mtu kuongea na mke wake katika simu na kuzungumza maongezi ya mapenzi kwani huyo ni halali yako, kwa hiyo hakuna tofauti ya kuongea naye kwa simu au unapokuwa naye.
Inapofika hali hiyo uliyoitaja ya baada ya mazungumzo na kutokwa na manii japo kuwa hukujimai naye mke wako, inakubidi ufanye Ghuslu na hii ni kutokana na dalili ya Hadiyth ifuatayo, kwamba Ummu Sulaym رضي الله عنها alimuendea Mtume صلى الله عليه وآله وسلم akamuambia:
"إن الله لا يستحي من الحق فهل على المرأة من غسل إذا هي احتلمت" فقال صلى الله عليه وسلم : " نعم إذا هي رأت الماء"
“Ewe Mtume wa Allah! Allah Haoni haya juu ya ukweli. Je, mwanamke inampasa afanye Ghuslu pindi akiota?" (Akiota ndoto ya kujimai) Akasema: “Ndio, anapoona maji” (Al-Bukhaariy na Muslim).
Kwa kupata maelezo zaidi kuhusu mas-ala haya tafadhali soma jibu la swali katika kiungo kifuatacho kwenye ALHIDAAYA:
Ikiwa Mtachezeana Tu Na Kutokwa Manii Inapasa Kukoga Josho?
Na Allaah Anajua zaidi.
- Login or register to post comments
- Email this page
- Chapisha


