Sherehe Za Kukaribisha Na Kuagana Wanafunzi Zinafaa?
SWALI:
Assalam Aleykum Warahmatullah Wabarakatu.
Naomba kupata ufafanuzi juu ya sherehe zinazo endeshwa na jumuiya za wanafunzi wa kiislamu je ni sahihi kwa mujibu wa mafundisho? Mfano sherehe za kuwaaga au kuwakaribisha wanafunzi kwa kuweka vyakula na vinywaji mbalimbali.
JIBU:
Sifa zote njema Anastahiki Allaah Aliyetukuka Mola Mlezi wa walimwengu wote, Swalah na salamu zimshukie kipenzi chetu Mtume Muhammad (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) na Swahaba zake (Radhiya Allaahu ‘anhum) na watangu wema mpaka Siku ya Mwisho.
Shukrani zetu za dhati kwa swali lako kuhusu sherehe zinazofanywa vyuoni kwa ajili ya kuwakaribisha wanafunzi au kuwaaga.
Sherehe hizo hazina tatizo katika Dini ikiwa zitafanywa kwa misingi ya Dini. Kuwepo na kuamrishana mema na kukataza maovu, kuusiana katika mema na kusiwepo mambo yoyote yale ya haramu.
Ni lazima kuwe na udhibiti wa kisheria
Na Allaah Anajua zaidi
- Login or register to post comments
- Email this page
- Chapisha
