Mkate Wa Shimari Na Zabibu

Mkate Wa Shimari Na Zabibu

 

 

 

Vipimo

 

Unga wa ngano                2 ½ Vikombe Vya chai

 

Siagi                                3 vijiko vya supu

 

Chumvi                           1 kijiko cha chai

 

Sukari                             1 kijiko cha supu

 

Hamira                            1 ½ vijiko vya chai

 

Bizari tamu (Shimari)       1 kijiko

 

Zabibu                             kiasi ukipenda

 

Yai                                   1

 

Rangi ya manjano             kidogo tu

 

Baking powder                1 kijiko cha chai

 

Maziwa                           1 kikombe cha chai

 

 

Namna Ya Kutayarisha Na Kupika

 

  1. Tia vitu vyote pamoja isipokuwa zabibu utatia kisha kanda.
  2. Kisha tia maziwa kidogo kidogo na huku ukikanda mpaka uwe laini kidogo utakuwa unashika.
  3. Halafu tia zabibu funika weka pembeni mpaka ufure (uumuke) kidogo.
  4. Kisha utauchanganya tena na utamimina kwenye sufuria na utautandaza kisha funika weka pembeni mpaka ufure zaidi.
  5. Halafu pakiza maziwa juu na choma kwenye oveni moto wa 350°c hadi iwive nakubadilika rangi juu.
  6. Epua na itakuwa tayari.

 

 

Share