Skip navigation.
Home kabah

Inajuzu Kufungua Hotel Ramadhaan?

SWALI:

Assalaam alaikum,

Swali langu linakuja kwenye uhalali wa kutoa huduma za kuuza chakula mchana wa mwezi Mtukufu wa ramadhani. Kama inafaa kutoa huduma hii naomba unipatie dalili zake ili nipate mwangaza zaidi juu ya jambo hili, na kama haifai naomba unifahamishe hukmu ya watu hawa wanaotoa huduma ya chakula mchana wa ramadhani kwa sababu za kuhudumia wagonjwa, wasafiri, wanawake walio katika tarehe zao na hata wasiokuwa waislam.

Nitafurahi iwapo nitajibiwa kabla ya mwezi wa ramadhani kwa faida ya walio wengi.

 

 



 

JIBU:

Sifa zote njema anastahiki Allah Aliyetukuka Mola Mlezi wa walimwengu wote, Swalah na salamu zimshukie kipenzi chetu Mtume Muhammad (Swalla Allahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) na Swahaba zake (Radhiya Allaahu 'anhum)  na watangu wema mpaka Siku ya Mwisho.

Shukrani zetu za dhati kwa wote wenye kuchangia au kuuliza maswali. Kuhusu hili jambo ni kuwa inategemea hali ilivyo na sehemu iliyopo kazi hiyo na hasa wakati wa Ramadhan. Ni yakini kuwa ikiwa tupo katika Dola ya Kiislamu yenye kuhukumiwa na Shari'ah tukufu, utawala huo hautaruhusu wenye mahoteli kuuza vyakula wakati wa mchana katika mwezi Mtukufu wa Ramadhan. Sababu ni kuwa kufanya huko kunaweza kuwashawishi Waislamu kuweza kuingia katika hoteli hizo na kula.

Mpaka wakati huu wetu wa leo tunaona kuwa miji ambayo Waislamu ni wengi hasa katika mwambao wa pwani wa Afrika Mashariki ikifika Ramadhan watu hufunga mahoteli yao kwa ajili ya ukarabati au hufungua karibu na magharibi. Hii ni ada au desturi ('Urf) ambayo imechukuliwa kama chimbuko la kisheria na Maimamu wakubwa kama Imaam Abu Hanifah na Maalik. Na desturi kama hii imeshikiliwa na hata wafuasi wengi wa Shaafi'iy katika sehemu hiyo tuliyoitaja hapo juu.

Hali nyengine ni kuwa mtu ni mfanya kazi hiyo lakini yupo katika mji au nchi ambao Waislamu ni kidogo kuliko wsiokuwa Waislamu. Hapa kunaweza kupatikana kama hali mbili. Ya kwanza ni kuwa ikiwa mtu mwenyewe ni mueza basi ni bora afunge hoteli yake mpaka Ramadhan imalizike. Ikiwa mfanya biashara mwenyewe hajiwezi na hilo ndio tegemeo lake la kuweza kujikimu na kuiweka familia yake katika hali nzuri basi anaweza kufungua hoteli yake kwa ajili ya kuwauzia wasiokuwa Waislamu, wasafiri hata ikiwa ni Waislamu. Na hatakuwa ni mwenye kuingia katika ubaya wowote.   

Na Allah Anajua zaidi