Ushindi Katika Ramadhaan
Imekusanywa Na: Muhammad Al-Ma'awy
UTANGULIZI
Mwezi wa Ramadhaan ni mwezi uliojaa juhudi na fadhila tele na nyingi ambazo lau zitatiliwa maanani, Ummah huu utanyanyuka kutoka daraja moja hadi nyengine. Huu ni mwezi wa Qur-aan, kwa kuwa iliteremshwa kwayo. Hivyo ni juu yetu kuisoma kwa kuzingatia na kufanyia kazi amri zilizotolewa ndani yake. Allah (Subhaanahu Wa Ta’ala) Anasema: “Ramadhaan ni mwezi ambao Qur-aan imeteremshwa ili iwe uongozi kwa watu, na hoja zilizo wazi wa uongozi na upambanuzi (wa baina ya haki na batili)” (2: 185).
Huu ni mwezi wa Usiku wa Qadari (wenye Nguvu – Laylatul Qadr), ambao usiku huo ni bora kuliko miezi elfu moja. Allah (Subhaanahu Wa Ta’ala) Anasema: “Laylatul Qadr ni bora kuliko miezi elfu moja” (97: 3).
Huu ndio mwezi wa Funga ya Faradhi, kwani Allah (Subhaanahu Wa Ta’ala) Anasema: “Enyi Mlioamini! Mmelazimishwa kufunga
Huu pia ndio mwezi wa Sadaka, ‘Umrah, Du’aa, Subira na Jihadi. Hii haimanishi miezi mingine huwa hivi vitu havifai kufanywa. Laa hasha! Maana yake ni kuwa katika mwezi wa Ramadhaan Muislamu anatakiwa aongeze amali hizi. Tufahamu ya kuwa huu sio mwezi wa kulala kupindukia au kula
MASHARTI YA USHINDI
Ushindi hauteremki kutoka katika ombwe wala haiji bila kutarajiwa. Ushindi na kushindwa zipo na kutawaliwa na kanuni na njia, ambazo zimenukuliwa na Allah (Subhaanahu Wa Ta’ala) katika Qur-aan ili Waumini waweze kuzijua kwa yakini, elimu ya uhakika na kwa upeo mkubwa zaidi. Kanuni hizi hazibadiliki kwa kiasi kikubwa. Allah (Subhaanahu Wa Ta’ala) Anasema yafuatayo kuhusu kanuni hizi: “Kabla yenu zimepita nyendo nyingi; basi tembeeni katika ulimwengu muangalie vipi ulikuwa mwisho wa wanaokanusha” (3: 137).
Na pia, “Hii ni ada ya Allah iliyokuwa kwa wale waliopita zamani. Wala hutapata mabadiliko katika ada ya Allah” (33: 62).
Na Anasema tena Aliyetukuka: “Huo ndio mwendo wa Allah uliokwishapita zamani, wala hutapata mabadiliko katika mwendo wa Allah” (48: 23).
Shida kubwa ya Ummah huu ambao unakumbana nao leo ni kuwa wafuasi wake (Waislam) wameleweshwa na kasumba za Kimagharibi na za kigeni, zilizopotoka kutoka katika njia nyoofu na wamesahau ujumbe wao. Tumeshindwa kutofautisha baina ya adui na rafiki na hatujui mikakati na njama dhidi yake na yetu). Hivyo, kwa Umma wowote kuweza kushinda dhidi ya adui yake masharti fulani ni lazima yapatikane. Ikiwa kipote kimoja au chochote kimeweza kutekeleza masharti hayo, ushindi utakuwa wao. Nyakati za ushindi na kushindwa zinabadilishana mikono kutegemea kanuni fulani. Allah (Subhaanahu Wa Ta’ala) Anasema: “
Masharti yenyewe yameelezwa hapa chini:
1. IMANI YENYE NGUVU
Imani ni sharti kwetu sisi kuweza kuwashinda makafiri. Ikiwa Waislam ni wakweli na Waumini wa kihakika basi wataweza kuwashinda maadui zao kila wakati na lau hatutaweza kuwa juu
Wakati mwengine Allah (Subhaanahu Wa Ta’ala) Anawatumia Malaika ili wawasaidie Waumini
Yeye (Subhaanahu Wa Ta’ala) Anasema tena: “Kisha Allah Akateremsha utulivu wake juu ya Mtume wake na juu ya Waumini. Na Akateremsha majeshi ambayo hamkuyaona, na Akawaadhibu wale waliokufuru. Na hayo ndiyo malipo ya makafiri” (9: 26).
Allah (Subhaanahu Wa Ta’ala) Anatumia njia nyengine yoyote Anayopenda kuwasaidia Waumini katika vita dhidi ya mushirikina
Sharti kubwa ya kushinda maadui ni kuwepo kwa pote la “Waumini”. Na lau Waumini watasimama imara basi Allah (Subhaanahu Wa Ta’ala) Atawafanya wao waweze kuitawala ardhi hii, ikitokea kinyume na
Waumini wanatakiwa kuwa na ufahamu na utambuzi na mas-ala kadhaa ya Uislamu. kwa huu ufahamu ina maana kuwa hata fikra zetu ziwe kwa ukamilifu wake zinakwenda sambamba na mambo yanayohusiana na maisha katika dunia hii. Katika haya Muumini anafaa afahamu mas-ala yafuatayo ambayo ni muhimu
· Tawhidi iliyo
· Kujua misingi na mambo muhimu ya Uislamu na kushikamana barabara na Qur-aan na Sunnah za kipenzi chetu Mtume Muhammad (swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam). Allah (Subhaanahu Wa Ta’ala) anasema: “Enyi mlioamini! Mtiini Allah, na mtiini Mtume na wenye madaraka katika nyinyi. Na mkizozana katika jambo basi lirudisheni kwa Allah na Mtume, ikiwa mnamuamini Allah na Siku ya Mwisho. Hayo ndiyo bora zaidi na ndiyo yenye mwisho mwema” (4: 59).
· Uoni (kuona mbali) na uangalifu katika kazi na shughuli za Da‘wah. Allah (Subhaanahu Wa Ta’ala) Anasema: “Sema: Hii ndiyo Njia yangu - ninalingania kwa Allah kwa kujua - mimi na wanaonifuata. Na ametakasika Allah! Wala mimi si katika washirikina” (12: 108).
· Kuwa na maadili madhubuti yenye kuigwa na wengine kwa sababu wewe umefuata kielelezo na ruwaza njema katika shakhsiya ya Mtume Muhammad (swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam). Tukiiga Akhlaaq za Mtume (swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) basi hatutapotea bali tutakuwa na ufanisi wa hapa duniani na pia Kesho akhera. Allah (Subhaanahu Wa Ta’ala) Anatuambia: “Hakika nyinyi mnayo ruwaza njema kwa Mtume wa Allah kwa anaye mtaraji Allah na Siku ya Mwisho, na akamkumbuka Allah
· Kutafuta elimu yote yenye manufaa kwa Ummah huu wa Kiislamu na kushindaa katika
· Kuweza kufuatilia habari za yanayojiri kila leo pamoja na kujua habari za Waislam katika nchi nyengine.
2. UKIMSAIDIA ALLAH, ATAKUSAIDIA
Hakika ni kuwa ushindi unakuja kutoka kwa Allah (Subhaanahu Wa Ta’ala). Yeyote anayesaidiwa na Allah (Subhaanahu Wa Ta’ala) hakuna hata mmoja wa kumshinda na kumpiku, japokuwa huenda wakawa wao ni wengi na wenye silaha kali na kubwa za kisasa. Allah (Subhaanahu Wa Ta’ala) Anasema: “Akikunusuruni Allah hapana wa kukushindeni, na Akikutupeni ni nani, basi, baada yake Yeye atayekunusuruni? Na Waumini wamtegemee Allah tu” (3: 160).
Allah (Subhaanahu Wa Ta’ala) Anawasaidia Waumini japokuwa watakuwa kidogo kama vile jeshi la Twaalut,
Hivyo ni kuwa yeyote mwenye kumsaidia Allah (Subhaanahu Wa Ta’ala), Allah (Subhaanahu Wa Ta’ala) Ametoa ahadi ya kumsaidia kwa msingi wa sharti hili. Allah (Subhaanahu Wa Ta’ala) Anasema: “Enyi mlioamini! Mkimnusuru Allah naye Atakunusuruni na Ataithibitisha miguu yenu” (47: 7).
3. KUSHIKAMANA VILIVYO NA UISLAMU
Kushikamana kikweli na kwa ikhlasi na Uislamu ni sharti katika kufaulu na kupata ushindi. Lau watu watapotoka kutoka kwa mafundisho ya Qur-aan na Sunnah basi wakati huo tutakumbwa na matatizo na shida aina zote mpaka tutakaporudi katika mafundisho ya Dini yetu, sahihi na
Utii kwa Allah (Subhaanahu Wa Ta’ala) na Mtume Wake (swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) ni muhimu
Sayyidna ‘Umar ibn al-Khatwtwaab (eadhiya Allaahu ‘anhu) amesema: “Sisi ni watu tuliopatiwa utukufu na nguvu na Allah (Subhaanahu Wa Ta’ala) kwa Uislamu, pindi tu tukapokengeuka (na kupotoka) na Uislamu basi hapo Allah (Subhaanahu Wa Ta’ala) Atatudhoofisha na kututweza”.
4. UONGOZI WENYE IKHLASI
Wakati ambapo tulikuwa na uongozi wenye ikhlasi na uchaji Mngu, Waislam waliendelea kuwashinda maadui zao kwa usahali
VITA WAKATI WA RAMADHAAN
Katika mwezi mtukufu wa Ramadhaan, Allah (Subhaanahu Wa Ta’ala) Aliwasaidia Waislam
Baadhi ya matukio ya kivita yaliyo muhimu ambayo yalitokea katika mwezi huu wa Ramadhaan wakati ambao Waislam waliweza kupata ushindi ni:
1. Vita vya Badr, vilivyopiganwa tarehe 17 Ramadhaan 2 H (624 Miladi): Waislam walikuwa 313 dhidi ya makafiri 1000. Mbali na idadi ndogo na maandalizi duni, waliweza kuwashinda mahasimu wao. Hivi ndivyo vilivyokuwa vita vya kwanza, ambavyo viliwafungulia Waislam silsila ya ushindi.
2. Maandalizi ya Vita vya Khandaq vilianza Ramadhaan ya mwaka wa 5 H (627 M). Matayarisho yalikuwa ni kufukuliwa kwa handaki katika pande tatu za mji wa Madinah ili kuwa ni kizuizi kwa makafiri waliojiandaa na kushirikiana.
3. Kufunguliwa kwa mji wa Makkah ambao ndio uliokuwa ushindi na ufanisi mkubwa wa Mtume (swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) dhidi ya mushirikina wa Makkah. Ushindi huu wa kuingia Makkah bila ya kumwagwa damu ulitokea 20 Ramadhaan 8 H (630 M).
4. Safari ya kuelekea Taabuk kwa Mtume (swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) na jeshi
5. Kufunguliwa na kutawaliwa kwa Maghrib al-Awswat (
6. Ufuo wa Pwani wa Andalus (
7. Amuriah ilitekwa tarehe 6 Ramadhaan 222 H.
8. Mujaahid Nuur ud Diyn Zinkiy aliwashinda Wakristo wa msalaba na kuurudisha mji Harem mnamo 9 Ramadhaan 559 H.
9. Sultan wa Misri wakati huo wake, Qitz Mahmuud Mudhaffar akiongoza jeshi waliokuwemo wanazuoni, vijana, wazee na hata wanawake, mkewe akiwemo ndani yake walipambana na Matatari ambao walikuwa wanatisha na kuogopewa. Hawa watu walivamia na kuiteka miji mingi katika dola ya Kiislamu pamoja na kumuua Khalifah wa Banu ‘Abbaas, mwaka 1258 M. Baghdad ambao ulikuwa ni mji mkuu wa dola hiyo ulivunjwa kabisa. Kwa hofu waliokuwa nayo Waislam walikuwa na msemo: “Ukisikia Matatari wameshindwa basi usisadiki”. Lakini walitokea waliowashinda watu hao majabari. Sultan Qitz na mujahidina wake walipambana na Matatari katika Vita vya ‘Ayn Jaalut huko Palestina tarehe 25 Ramadhaan 658 H (1260 M) miaka miwili pekee baada ya kuuliwa kwa Khalifa. Qitz alinyanyua hima na hamasa ya mujahidina wake. Chini ya uongozi wake, Waislam walishikanishwa juu ya Imani, umoja, zana za kivita za chuma ili kupambana na adui. Matokeo yake yalikuwa ni ushindi wa wazi kabisa katika wakati wa udhaifu na unyonge. Hata leo tunaweza kupata ushindi na aina hiyo ya uongozi. Kadhiya ya
10. Ndugu zetu huko
11. Ukinzani na mapigano dhidi ya maadui wa Uislamu bado yanaendelea kwa miongo kadhaa katika nchi kama Palestina, Kashmir,
12. Vita vya Ramadhaan 1973 baina ya majeshi ya Kiarabu na Waisraeli imeonyesha kuwa lau nchi za Mashariki ya Kati zitashikana mikono na kuungana kwa ikhlasi na kupigana dhidi ya adui kwa ajili ya Allah basi adui atatoka mwenyewe katika eneno
Lakini wakati masharti ya kupata ushindi yalikosekana Waislam walishindwa katika mwezi huo mtukufu wa Ramadhaan. Mojawapo ya kushindwa vibaya
HITIMISHO
Kwetu sisi kutoka katika janga hili la balaa inafaa tuwe na suluhisho, la sivyo shida na matatizo yatazidi. Kwa mtazamo wa haraka ni kuwa mustakabali katika hii dunia ni kwa Uislamu hata wakichukia makafiri, lakini majukumu ni lazima yabebwe na kila mmoja wetu. Kila mmoja wetu anafaa kucheza dauru yake ili kuweza kufikia malengo yetu. Hili ni lazima lichukuliwe
Mabadiliko ni lazima yaanze
“Hakika Allah Habadili yaliyoko kwa watu mpaka wabadili wao yaliyomo nafsini mwao” (13: 11). Njia ya sisi kwenda mbele ni kufuatilia muongozo ufuatao:
1. Mazoezi ya Kimwili: Allah (Subhaanahu Wa Ta’ala) Anatueleza kwamba: “Basi waandalieni nguvu
Na Mtume wa Allah (swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) anatuambia: “Muumini aliye na nguvu ni bora na anapendwa zaidi na Allah kuliko Muumini aliye dhaifu” (Muslim). Hata wanawake hawakuachwa nyuma katika mas-ala haya ya kujiweka katika hali ya maandalizi na mazoezi. Wakati mmoja ‘Aaishah (radhiya Allaahu ‘anha) alishindana mbio na Mtume (swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) naye akashinda (Ahmad na Abu Daawuud). Hivyo, ni muhimu
2. Mazoezi ya Kiroho: Ni muhimu kwa Waislam kujitolea mhanga kwa ajili ya kuzisafisha nyoyo zao kwa kusoma, kujua maana na kuzingatia maamrisho yaliyomo ndani ya Qur-aan pamoja na kushikamana barabara na Sunnah. Ni lazima walime na kupalilia ndani ya nafsi zao hisia ya kutekeleza ‘Ibadah kwa mfano Swalah, Funga, Dhikr na aina nyengine za ‘Ibadah ambazo zitatuleta sisi karibu na Allah (Subhaanahu Wa Ta’ala) za faradhi na za Sunnah. Hii itaitakasa na kuisafisha roho zetu. Jambo hili linatakiwa lipatiwe umuhimu mkubwa kabisa.
3. Mazoezi ya Kiakili: Ikiwa ni katika Misikiti au katika vyuo vya masomo Waislam wanatakiwa wajengwe kiakili. Akili zao zinatakiwa zifunguliwe na masikio
Wabillahi at-Tawfiq
- Login or register to post comments
- Email this page
- Chapisha
