Ramadhaan-Swawm

Ramadhaan-Swawm

Ramadhaan-Swawm

Nini Baada Ya Ramadhwaan?

Alhidaaya.com

 

Tumeuaga mwezi wa Ramadhwaan, mwezi wenye Baraka na Rahmah. Tumeaga mchana wake tulipokuwa katika subira ya Swawm, na usiku wake tulipoonja ladha ya Qiyaamul-Layl (kusimama usiku kuswali). Tumeuaga mwezi wa Qur-aan, mwezi wa taqwa, mwezi wa jihaad, mwezi wa maghfirah, mwezi wa kuomba du'aa kwa wingi, mwezi wa kuepushwa na Moto. Amefaulu aliyetimiza Swiyaam ilivyopaswa akachuma thawabu nyingi na akajitahidi kuzidisha ‘ibaadah. Lakini amekula hasara aliyepuuza Swiyaam na hukmu zake na kutokujitahidi katika ‘ibaadah.    

 

Kama Anavyosema Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa) katika Aayah zilizofaridhishwa kufunga Swiyaam katika Ramadhwaan kuwa lengo la Swiyaam ni taqwa.

يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا كُتِبَ عَلَيْكُمُ الصِّيَامُ كَمَا كُتِبَ عَلَى الَّذِينَ مِن قَبْلِكُمْ لَعَلَّكُمْ تَتَّقُونَ ﴿١٨٣﴾

Enyi walioamini! Mmefaridhishwa Swiyaam kama ilivyoandikwa kwa wale ambao wa kabla yenu mpate kuwa na taqwa [Al-Baqarah: 183]

 

Kila Muislamu aliyeingia katika mwezi wa Ramadhwaan atakuwa ameingia na ametoka katika madrasa ya taqwa. Na mtu anapoingia katika madrasa yoyote ile, hutoka humo akiwa amepata manufaa au shahada ya lile somo alilolisoma, na baada ya hapo...

 

Bonyeza Endelea...

 

 

Ramadhaan-Swawm

 

Mambo Matatu Yanayofuatia Ramadhwaan:

 

Zakaatul-Fitwr, 'Iydul-Fitwr Na Swawm Ya Sitta  Shawwaal

 

www.alhidaaya.com

 

 

Tunakaribia kumaliza mwezi mtukufu wa Ramadhwaan na mambo matatu yafuatayo ya muhimu yanayotukabili yanapasa kuzingatiwa ili tukamilishe Swawm zetu ipasavyo na tupate fadhila zake.

 

1.Zakaatul-Fitwr:

 

Inaitwa Zakaatul-Fitwr (Zakaah ya Kufuturu au Kufutari) kutokana na kumalizika Swiyaam za Ramadhwaan. Imefaridhiwa mwaka wa pili wa Hijrah katika mwezi wa Ramadhwaan.

 

i-Hikmah Ya Zakaatul-Fitwr:

 

Zakaatul-Fitwr ni kwa ajili ya kutakasa Swiyaam za Muislamu kutokana na maneno machafu na ya upuuzi wakati alipokuwa katika Swawm kwa kulisha maskini chakula ili nao wapate chakula kizuri siku ya ‘Iyd. Ndio maana kutolewa kwake kunakuwa kabla ya kuswali Swalaah ya ‘Iydul-Fitwr kwa dalili zifuatazo:

 

Tafadhali bonyeza viungo vifuatavyo  kuhusu Fataawaa za Zakaatul-Fitwr:

 

 

 

 

 

Bonyeza Endelea...

 

 

Ramadhaan-Swawm

Laylatul-Qadr- Vipi Uweze Kuupata Usiku Huu?

Imekusanywa Na:  Alhidaaya.com

 

 

Tunaingia kumi la mwisho la Ramadhwaan, kumi ambalo ndani yake kuna Laylatul-Qadr. ‘ibaadah yoyote itakayotendwa usiku huo, ni bora kuliko ‘ibaadah ya miezi elfu.

 

Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

بِسْمِ اللَّـهِ الرَّحْمَـٰنِ الرَّحِيمِ

إِنَّا أَنزَلْنَاهُ فِي لَيْلَةِ الْقَدْرِ ﴿١﴾

Hakika Sisi Tumeiteremsha Qur-aan katika Laylatil-Qadr (usiku wa Qadar).

وَمَا أَدْرَاكَ مَا لَيْلَةُ الْقَدْرِ ﴿٢﴾

Na nini kitakachokujulisha ni nini huo Laylatul-Qadr?

لَيْلَةُ الْقَدْرِ خَيْرٌ مِّنْ أَلْفِ شَهْرٍ ﴿٣﴾

Laylatul-Qadr ni mbora kuliko miezi elfu.

تَنَزَّلُ الْمَلَائِكَةُ وَالرُّوحُ فِيهَا بِإِذْنِ رَبِّهِم مِّن كُلِّ أَمْرٍ ﴿٤﴾

Wanateremka humo Malaika na Ar-Ruwh (Jibriyl) kwa idhini ya Rabb wao kwa kila jambo.

سَلَامٌ هِيَ حَتَّىٰ مَطْلَعِ الْفَجْرِ ﴿٥﴾

Amani mpaka kuchomoza Alfajiri.    [Al-Qadr: 1-5]

 

Hadiyth mbali mbali zimethibiti kuhusu fadhila za usiku huu mtukufu na jinsi Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alivyokuwa katika masiku kumi ya mwisho ya Ramadhwaan.

 

Hesabu ya thawabu za usiku huo ni kama ifuatavyo:

 

Bonyeza Endelea...

 

Ramadhaan-Swawm

Ramadhwaan Ni Mwezi Wa Du’aa Na Du’aa Hutakabaliwa

 

Alhidaaya.com

 

 

Du’aa ni ‘ibaadah kama ilivyothibiti katika Hadiyth:

 

 

عَنِ النُّعْمَانِ بْنِ بَشِيرٍ (رضي الله عنه) عَنْ النَّبِيِّ (صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ) فِي قَوْلِهِ ((وَقَالَ رَبُّكُمُ ادْعُونِي أَسْتَجِبْ لَكُمْ)) قَالَ: ((الدُّعَاءُ هُوَ الْعِبَادَةُ)) وَقَرَأَ ((وَقَالَ رَبُّكُمُ ادْعُونِي أَسْتَجِبْ لَكُمْ)) إِلَى قَوْلِهِ: ((دَاخِرِينَ))

Amesimulia Nu’maan bin Bashiyr (رضي الله عنه) kwamba Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) kuhusu kauli yake [Allaah Subhaanahu wa Ta’aalaa]: 

وَقَالَ رَبُّكُمُ ادْعُونِي أَسْتَجِبْ لَكُمْ

((Na Rabb wenu Amesema: “Niombeni, Nitakuitikieni))

 

Amesema: ((Du’aa ndio ‘ibaadah)) kisha akasoma: 

 

وَقَالَ رَبُّكُمُ ادْعُونِي أَسْتَجِبْ لَكُمْ ۚ إِنَّ الَّذِينَ يَسْتَكْبِرُونَ عَنْ عِبَادَتِي سَيَدْخُلُونَ جَهَنَّمَ دَاخِرِينَ﴿٦٠﴾

Na Rabb wenu Amesema: Niombeni, Nitakuitikieni. Hakika wale wanaotakabari katika kuniabudu wataingia Jahanam wadhalilike.  [Ghaafir: 60] [Abu Daawuwd, At-Tirmidhiy, Ibn Maajah, Ahmad – Hadiyth Hasan Swahiyh]

 

Juu ya hivyo, du’aa ni ‘amali tukufu kabisa mbele ya Allaah (سبحانه وتعالى):

 

عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ (رَضِيَ اللَّهُ عَنْهُ) عَنْ النَّبِيِّ (صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ) قَالَ: ((لَيْسَ شَيْءٌ أَكْرَمَ عَلَى اللَّهِ تَعَالَى مِنْ الدُّعَاءِ))  

Kutoka kwa Abu Hurayrah (رضي الله عنه) kwamba Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم)    amesema: ((Hakuna kitu kitukufu mbele ya Allaah kama du’aa))  [Swahiyh Adab Al-Mufrad]

 

Na Allaah (سبحانه وتعالى) Ameiadhimisha ‘amali ya kuomba du’aa khasa katika mwezi wa Ramadhwaan kwa sababu zifuatazo: