Kamba Wa Kuchomwa Katika Mkaa BBQ

Kamba Wa  Kuchomwa Katika Mkaa  BBQ

  

    

Mahitajio

Utayarishaji

Kipimo

 

Kamba wakubwa

osha chuja maji

2 kilo

Pilipili boga/Capsicum

katakata vipande kiasi

5- 10 

Nyanya/tungule ndogo ndogo

osha tu weka kando

15-20

Ukwaju wa brauni

roweka, kamua

2 vikombe vya chai

chumvi

 

kiasi

pilipili nyekundu ya unga

 

1 kijiko cha supu

pilipili mbichi ya kijani/ya shamba

saga

7

Bizari ya pilau/cummin

ilosagwa

2 vijiko vya chai

Vijiti vya BBQ

 

kiasi

 

Namna Ya Kupika:

  1. Weka kamba katika bakuli.
  2. Changanya ukwaju, chumvi, pilipili zote, bizari katika kibakuli.
  3. Tia sosi ya ukwajui katika kamba changanya vizuri, acha kando kuwaroweka wakolee vizuri. Weka kiasi muda wa masaa mawili au zaidi.
  4. Chomeka kamba katika vijiti kwa kuweka baina yake tungule/nyanya na kipande cha pilipili boga
  5. Choma katika mkaa huku unarashia sosi ilobakia katika bakuli.

 

 

 

 

 

 

 

Share