051 - Adh-Dhaariyaat
الذَّارِيَات
Adh-Dhaariyaat: 051
بِسْمِ اللَّـهِ الرَّحْمَـٰنِ الرَّحِيمِ
وَالذَّارِيَاتِ ذَرْوًا﴿١﴾
1. Naapa kwa (pepo) zinazopeperusha vumbi kuzitawanya.
فَالْحَامِلَاتِ وِقْرًا﴿٢﴾
2. Kisha Naapa kwa (mawingu) yanayobeba mzigo wa maji.
فَالْجَارِيَاتِ يُسْرًا﴿٣﴾
3. Kisha Naapa kwa (merikebu) zinazotembea kwa wepesi.
فَالْمُقَسِّمَاتِ أَمْرًا﴿٤﴾
4. Kisha Naapa kwa (Malaika) wenye kugawanya amri.
إِنَّمَا تُوعَدُونَ لَصَادِقٌ﴿٥﴾
5. Hakika mnayoahidiwa bila shaka ni kweli.
وَإِنَّ الدِّينَ لَوَاقِعٌ﴿٦﴾
6. Na hakika malipo bila shaka yatatokea.
وَالسَّمَاءِ ذَاتِ الْحُبُكِ﴿٧﴾
7. Naapa kwa mbingu zilizojaa njia madhubuti.
إِنَّكُمْ لَفِي قَوْلٍ مُّخْتَلِفٍ﴿٨﴾
8. Hakika nyinyi bila shaka mko katika kauli inayokhitilafiana.
يُؤْفَكُ عَنْهُ مَنْ أُفِكَ﴿٩﴾
9. Ameghilibiwa kwayo anayeghilibiwa (kuhusu haki).
قُتِلَ الْخَرَّاصُونَ﴿١٠﴾
10. Wameangamia wanaobuni uongo.
الَّذِينَ هُمْ فِي غَمْرَةٍ سَاهُونَ﴿١١﴾
11. Ambao wamo katika mfuniko wa mghafala, wenye kupurukusha (kuhusu Aakhirah).
يَسْأَلُونَ أَيَّانَ يَوْمُ الدِّينِ﴿١٢﴾
12. Wanauliza: Lini hiyo Siku ya malipo?
يَوْمَ هُمْ عَلَى النَّارِ يُفْتَنُونَ﴿١٣﴾
13. Siku wao watakapoteswa motoni.
ذُوقُوا فِتْنَتَكُمْ هَـٰذَا الَّذِي كُنتُم بِهِ تَسْتَعْجِلُونَ﴿١٤﴾
14. Onjeni adhabu yenu. Haya ndiyo ambayo mlikuwa mkiyahimiza.
إِنَّ الْمُتَّقِينَ فِي جَنَّاتٍ وَعُيُونٍ﴿١٥﴾
15. Hakika wenye taqwa watakuwa katika Jannaat na chemchemu.
آخِذِينَ مَا آتَاهُمْ رَبُّهُمْ ۚ إِنَّهُمْ كَانُوا قَبْلَ ذَٰلِكَ مُحْسِنِينَ﴿١٦﴾
16. Wakichukua yale Atakayowapa Rabb wao. Hakika wao walikuwa kabla ya hapo ni wahisani.
كَانُوا قَلِيلًا مِّنَ اللَّيْلِ مَا يَهْجَعُونَ﴿١٧﴾
17. Walikuwa kidogo tu katika usiku wakilala kwa raha.
وَبِالْأَسْحَارِ هُمْ يَسْتَغْفِرُونَ﴿١٨﴾
18. Na kabla ya Alfajiri wakiomba Maghfirah.
وَفِي أَمْوَالِهِمْ حَقٌّ لِّلسَّائِلِ وَالْمَحْرُومِ﴿١٩﴾
19. Na katika mali zao kuna haki maalumu kwa mwenye kuomba na asiyeomba.
وَفِي الْأَرْضِ آيَاتٌ لِّلْمُوقِنِينَ﴿٢٠﴾
20. Na katika ardhi kuna ishara kwa wenye yakini.
وَفِي أَنفُسِكُمْ ۚ أَفَلَا تُبْصِرُونَ﴿٢١﴾
21. Na katika nafsi zenu, je hamuoni?
وَفِي السَّمَاءِ رِزْقُكُمْ وَمَا تُوعَدُونَ﴿٢٢﴾
22. Na katika mbingu kuna riziki yenu na yale mnayoahidiwa.
فَوَرَبِّ السَّمَاءِ وَالْأَرْضِ إِنَّهُ لَحَقٌّ مِّثْلَ مَا أَنَّكُمْ تَنطِقُونَ﴿٢٣﴾
23, Basi Naapa kwa Rabb wa mbingu na ardhi, hakika hiyo ni haki kama nyinyi mnavyotamka.
هَلْ أَتَاكَ حَدِيثُ ضَيْفِ إِبْرَاهِيمَ الْمُكْرَمِينَ﴿٢٤﴾
24. Je, imekufikia hadithi ya wageni wahishimiwao wa Ibraahiym?
إِذْ دَخَلُوا عَلَيْهِ فَقَالُوا سَلَامًا ۖ قَالَ سَلَامٌ قَوْمٌ مُّنكَرُونَ﴿٢٥﴾
25. Walipoingia kwake wakasema: Salaam! Akasema: Salaam watu wasiotambulikana.
فَرَاغَ إِلَىٰ أَهْلِهِ فَجَاءَ بِعِجْلٍ سَمِينٍ﴿٢٦﴾
26. Akaondoka bila kuhisiwa kuelekea kwa ahli yake, akaleta ndama aliyenona.
فَقَرَّبَهُ إِلَيْهِمْ قَالَ أَلَا تَأْكُلُونَ﴿٢٧﴾
27. Akawakurubishia pale walipo, akasema: Mbona hamli?
فَأَوْجَسَ مِنْهُمْ خِيفَةً ۖ قَالُوا لَا تَخَفْ ۖ وَبَشَّرُوهُ بِغُلَامٍ عَلِيمٍ﴿٢٨﴾
28. Akawaogopa ndani ya nafsi yake. Wakasema: Usikhofu! Na wakambashiria ghulamu mjuzi.
فَأَقْبَلَتِ امْرَأَتُهُ فِي صَرَّةٍ فَصَكَّتْ وَجْهَهَا وَقَالَتْ عَجُوزٌ عَقِيمٌ﴿٢٩﴾
29. Mkewe akawakabili kwa ukelele wa furaha, akajipiga usoni na kusema: Kikongwe, tasa!
قَالُوا كَذَٰلِكِ قَالَ رَبُّكِ ۖ إِنَّهُ هُوَ الْحَكِيمُ الْعَلِيمُ﴿٣٠﴾
30. Wakasema: Hivyo ndivyo Alivyosema Rabb wako. Hakika Yeye Ndiye Mwenye Hikmah wa yote, Mjuzi wa yote.
قَالَ فَمَا خَطْبُكُمْ أَيُّهَا الْمُرْسَلُونَ ﴿٣١﴾
31. (Ibraahiym) akasema: Basi nini shughuli yenu mloikusudia enyi Wajumbe?
قَالُوا إِنَّا أُرْسِلْنَا إِلَىٰ قَوْمٍ مُّجْرِمِينَ ﴿٣٢﴾
32. Wakasema: Hakika sisi tumetumwa kwa watu wahalifu.
لِنُرْسِلَ عَلَيْهِمْ حِجَارَةً مِّن طِينٍ ﴿٣٣﴾
33. Ili Tuwavurumishie mawe ya udongo.
مُّسَوَّمَةً عِندَ رَبِّكَ لِلْمُسْرِفِينَ ﴿٣٤﴾
34. Yaliyotiwa alama kutoka kwa Rabb wako kwa wapindukao mipaka.
فَأَخْرَجْنَا مَن كَانَ فِيهَا مِنَ الْمُؤْمِنِينَ ﴿٣٥﴾
35. Basi Tukawatoa humo wale waliokuwa Waumini.
فَمَا وَجَدْنَا فِيهَا غَيْرَ بَيْتٍ مِّنَ الْمُسْلِمِينَ ﴿٣٦﴾
36. Lakini Hatukukuta humo isipokuwa nyumba moja tu ya Waislamu.
وَتَرَكْنَا فِيهَا آيَةً لِّلَّذِينَ يَخَافُونَ الْعَذَابَ الْأَلِيمَ ﴿٣٧﴾
37. Na Tukaacha humo athari kwa wale wanaoogopa adhabu iumizayo.
وَفِي مُوسَىٰ إِذْ أَرْسَلْنَاهُ إِلَىٰ فِرْعَوْنَ بِسُلْطَانٍ مُّبِينٍ ﴿٣٨﴾
38. Na kwa Muwsaa (pia ipo athari), Tulipomtuma kwa Firawni na Miujiza bayana.
فَتَوَلَّىٰ بِرُكْنِهِ وَقَالَ سَاحِرٌ أَوْ مَجْنُونٌ ﴿٣٩﴾
39. Akakengeuka (akitegemea nguvu) na askari na wasaidizi wake akasema: Mchawi au majnuni.
فَأَخَذْنَاهُ وَجُنُودَهُ فَنَبَذْنَاهُمْ فِي الْيَمِّ وَهُوَ مُلِيمٌ ﴿٤٠﴾
40. Tukamchukuwa na jeshi lake, kisha Tukawavurumisha katika bahari nailhali yeye ni mwenye kujiletea mwenyewe lawama.
وَفِي عَادٍ إِذْ أَرْسَلْنَا عَلَيْهِمُ الرِّيحَ الْعَقِيمَ ﴿٤١﴾
41. Na kwa kina ‘Aad, Tulipowapelekea upepo wa adhabu, mkame.
مَا تَذَرُ مِن شَيْءٍ أَتَتْ عَلَيْهِ إِلَّا جَعَلَتْهُ كَالرَّمِيمِ ﴿٤٢﴾
42. Haukuacha chochote ulichokifikia ila ulikifanya kama kilichobungulika na kuoza.
وَفِي ثَمُودَ إِذْ قِيلَ لَهُمْ تَمَتَّعُوا حَتَّىٰ حِينٍ ﴿٤٣﴾
43. Na kwa kina Thamuwd walipoambiwa: Stareheni kwa muda.
فَعَتَوْا عَنْ أَمْرِ رَبِّهِمْ فَأَخَذَتْهُمُ الصَّاعِقَةُ وَهُمْ يَنظُرُونَ ﴿٤٤﴾
44. Wakafanya ufidhuli kuhusu Amri ya Rabb wao, basi ikawachukuwa radi na umeme angamizi na huku wao wanatazama.
فَمَا اسْتَطَاعُوا مِن قِيَامٍ وَمَا كَانُوا مُنتَصِرِينَ ﴿٤٥﴾
45. Basi hawakuweza kusimama na wala hawakuwa wenye kujinusuru.
وَقَوْمَ نُوحٍ مِّن قَبْلُ ۖ إِنَّهُمْ كَانُوا قَوْمًا فَاسِقِينَ ﴿٤٦﴾
46. Na watu wa Nuwh hapo kabla. Hakika wao walikuwa kaumu mafasiki.
وَالسَّمَاءَ بَنَيْنَاهَا بِأَيْدٍ وَإِنَّا لَمُوسِعُونَ ﴿٤٧﴾
47. Na mbingu Tumezijenga kwa nguvu na qudra, na hakika Sisi Ndio Wenye Kupanua.
وَالْأَرْضَ فَرَشْنَاهَا فَنِعْمَ الْمَاهِدُونَ ﴿٤٨﴾
48. Na ardhi Tumeitandaza, basi Wazuri Tulioje Sisi wa Kutayarisha!
وَمِن كُلِّ شَيْءٍ خَلَقْنَا زَوْجَيْنِ لَعَلَّكُمْ تَذَكَّرُونَ ﴿٤٩﴾
49. Na kila kitu Tumeumba jozi mbili; dume na jike ili mpate kukumbuka.
فَفِرُّوا إِلَى اللَّـهِ ۖ إِنِّي لَكُم مِّنْهُ نَذِيرٌ مُّبِينٌ ﴿٥٠﴾
50. Basi kimbilieni kwa Allaah. Hakika mimi kwenu ni mwonyaji bayana kutoka Kwake.
وَلَا تَجْعَلُوا مَعَ اللَّـهِ إِلَـٰهًا آخَرَ ۖ إِنِّي لَكُم مِّنْهُ نَذِيرٌ مُّبِينٌ ﴿٥١﴾
51. Na wala msifanye pamoja na Allaah mwabudiwa mwingine, hakika mimi kwenu ni mwonyaji bayana kutoka Kwake.
كَذَٰلِكَ مَا أَتَى الَّذِينَ مِن قَبْلِهِم مِّن رَّسُولٍ إِلَّا قَالُوا سَاحِرٌ أَوْ مَجْنُونٌ ﴿٥٢﴾
52. Ndio kama hivyo, hawakuwafikia wale wa kabla yao Rasuli yeyote isipokuwa walisema: Mchawi au majnuni.
أَتَوَاصَوْا بِهِ ۚ بَلْ هُمْ قَوْمٌ طَاغُونَ ﴿٥٣﴾
53. Je, wameusiana kwa hayo? Bali wao ni watu wenye kupindukia mipaka ya kuasi.
فَتَوَلَّ عَنْهُمْ فَمَا أَنتَ بِمَلُومٍ ﴿٥٤﴾
54. Basi jitenge nao (ee Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم), kwani wewe si mwenye kulaumiwa kabisa.
وَذَكِّرْ فَإِنَّ الذِّكْرَىٰ تَنفَعُ الْمُؤْمِنِينَ ﴿٥٥﴾
55. Na kumbusha, kwani hakika ukumbusho unawafaa Waumini.
وَمَا خَلَقْتُ الْجِنَّ وَالْإِنسَ إِلَّا لِيَعْبُدُونِ ﴿٥٦﴾
56. Na Sikuumba majini na wana Aadam isipokuwa waniabudu.
مَا أُرِيدُ مِنْهُم مِّن رِّزْقٍ وَمَا أُرِيدُ أَن يُطْعِمُونِ ﴿٥٧﴾
57. Sitaki kutoka kwao riziki yoyote, na wala Sitaki wanilishe.
إِنَّ اللَّـهَ هُوَ الرَّزَّاقُ ذُو الْقُوَّةِ الْمَتِينُ ﴿٥٨﴾
58. Hakika Allaah Ndiye Mwingi wa Kuruzuku, Mwenye Nguvu Madhubuti.
فَإِنَّ لِلَّذِينَ ظَلَمُوا ذَنُوبًا مِّثْلَ ذَنُوبِ أَصْحَابِهِمْ فَلَا يَسْتَعْجِلُونِ ﴿٥٩﴾
59. Basi hakika wale waliodhulumu watakuwa na sehemu ya adhabu kama sehemu ya adhabu ya wenzao, basi wasihimize.
فَوَيْلٌ لِّلَّذِينَ كَفَرُوا مِن يَوْمِهِمُ الَّذِي يُوعَدُونَ ﴿٦٠﴾
60. Basi ole kwa wale waliokufuru kutokana na Siku yao ambayo wanaahidiwa.
