Samaki Wa Changu Wa Kukaanga

Samaki Wa Changu Wa Kukaanga

 

 

 

 

 

 

 

Vipimo 

Samaki changu - 3 wa kiasi                                                    

Bizari mchuzi - 2 vijiko cha supu

Pilipili nyekundu ya unga - 1 kijiko cha chai

Ndimu - 2 kamua

Chumvi - kisia

Mafuta ya kukaangia - kiasi                                        

Namna Ya Kutayarisha Na Kupika   

  1. Osha samaki mchuje maji.
  2. Changanya bizari, chumvi, pilipili na ndimu.
  3. Mpakaze samaki vizuri kisha mwache muda akolee viungo.
  4. Kaanga katika mafuta ya moto ugeuze mpaka ageuka rangi,
  5. Weka katika sahani tolea kwa mhogo, ndizi mbichi, wali wa nyanya au upendavyo.

Bis-swihhah wal-hanaa (kula kwa siha na kufurahika)

 

 

 

 

Share