Choroko Za Kupaaza Za Nazi

Vipimo
Choroko za kupaaza 1 kikombe kikubwa (mug)
Kitunguu maji 1 kimoja
Binzari ya manjano ya unga 1/2 kijiko cha chai
Vitungu saumu 1 kijiko cha chai
Nyanya 1 moja
Pilipili nzima 1-2
Chumvi kiasi
Nazi 1 kikopo (400-500 mls)
Namna Ya Kutayarisha
1. Osha choroko zako vizuri na zichemshe kwa maji ya kiasi tu hadi ziwive na zisivurugike.
2. Katakata kitunguu maji vipande vidogodogo.
3. Imenye nyanya maganda halafu iponde.
Namna Ya Kupika
1. Weka sufuria jikoni na moto wa kiasi tia mafuta kidogo.(kijiko kikubwa cha kulia)
2. Kaanga vitunguu mpaka vibadilike rangi kidogo
3. Tia binzari ya manjano kaangia kidogo
4. Kisha tia vitunguu thaumu kaanga kidogo.
5. Halafu mimina nyanya iliyosagwa na chumvi kiasi.
6. Acha ikaangike huku ukikoroga.(
7. Kisha mimina choroko zilizoshemshwa changanya acha maji yakauke kiasi
8. Mimina nazi na onja chumvi
9. Mwisho katia pilipili ziwivie kiasi.
Zikisha kuwa tayari mimina kwenye bakuli lako tayari kwa kuliwa na chapati , wali hata pita bread (mkate)
- Login or register to post comments
- Email this page
- Chapisha


