Kastadi Za Biskuti

VIPIMO
Mayai 2
Maji 3 Gilasi
Unga wa ngano 3 Vijiko vya supu
Nido (maziwa ya unga) 2 gilasi
Sukari 1/2 - 3/4 gilasi
Biskuti za Marie
Chokoleti
Vanilla Kiasi
NAMNA YA KUTAYARISHA NA KUPIKA
1. Tia maji kwanza kwenye blenda pamoja na hivyo vyote; na iache ichanganyikane vizuri.
2. Kisha tia mchanganyiko kwenye sufuria na tumia mwiko ukoroge moto mdogo na upike mpaka ishikane
3. Kisha twaa bakuli utie nusu ya hiyo kastadi upange biskuti kati kati halafu utie nusu nyingine ya hiyo kastadi juu ya hizo biskuti na kisha kwaruzia chokoleti juu yake.
4. Iache iwe baridi kisha pakuwa kwenye vibakuli na itakuwa tayari kuliwa.
KIDOKEZO:
- Login or register to post comments
- Email this page
- Chapisha


