Khalyat-An-Nahl (Mzinga Wa Nyuki)-1

Khalyat An-Nahl  (Mzinga Wa Nyuki)-1

 

 

Vipimo

Unga - Vikombe 3 ½ visivyojaa

Maziwa ya maji - Vikombe 1

Maji - Kikombe ½

Yai - 1

Sukari - Vijiko 2 ½ vya supu

Mafuta - Kikombe ½

Hamira - Kijiko ½ cha chai

Chumvi - robo kijiko cha chai

Cheese ya Cream - Kiasi utakavyotumia kujaza

 

Shira

 

Sukari - Vikombe 2

Maji - Kikombe 1 ½

Zaafarani - nusu kijiko cha chai (iroweke)

Ipikie shira lakini isiwe nzito. 

 

Namna Ya Kutayarisha Na Kupika

  1. Changanya vitu vyote hivyo isipokuwa cream cheese.
  2. Kanda kidogo tu kulainisha unga uwe mlaini kama mfano unga  wa maandazi. 
  3. Pakaza siagi katika sinia ya round utakayopikia 
  4. Fanya viduara vidogo vidogo na tia ndani yake cheese ya cream kwa kutumia kijiko cha chai, na vifunge viduwara vizuri na kuvipanga katika sinia  bila ya kuwacha nafasi.
  5. Iwache ifure
  6. Ipikie katika oven moto wa chini kwanza katika 350 Deg, kwa muda wa baina dakika  20  na 25 .  Kisha washa moto wa juu kidogo tu uwive kwa juu.
  7. Toa katika oven na mwagia shira kama ifuatavyo.

   

Vidokezo:

 

Kama ni shira iliyopowa basi mwagia juu ya mkate uliomoto

  

Kama ni shira imoto basi subiri mkate upowe.  Yaani mojawapo iwe moto au baridi.

 

 

Share