Anaweza Kufuta Picha Za Ngono Katika Kompyuta Ya Mwenziwe Bila ya Ruhusa?
SWALI
hongereni kwa program hii nimeikubali Allaah awazidishie mtoe bora zaidi ya hivi KEEP IN TOUCH MY FELLOW MUSLIMS je kuna tatizo lolote kufuta ie delete mambo ya kipuuzi like phonographs kwenye computer ya mtu bila ya kumtaarifu muhusika ie mwenye computer au bila yeye mwenyewe kukuruhusu sorry for this question if not good for you.
JIBU:
Sifa zote njema Anastahiki Allaah Aliyetukuka Mola Mlezi wa walimwengu wote, Swalah na salamu zimshukie kipenzi chetu Mtume Muhammad (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) na Swahaba zake (Radhiya Allaahu 'anhum) na watangu wema mpaka Siku ya Mwisho.
Shukrani zetu za dhati kwa swali lako ndugu yetu. Hakika ni kuwa Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala) na Mtume Wake (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) wametuhimiza
"Waite waelekee kwenye Njia ya Mola wako Mlezi kwa hekima na mawaidha mema, na ujadiliane nao kwa namna iliyo bora" (16: 125).
Na Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema:
"Yeyote katika nyinyi atakayeona munkari naubadilishe kwa mkono wake; na akiwa hawezi basi afanye hivyo kwa ulimi wake; na akiwa hawezi basi afanye kwa moyo wake na huo ni udhaifu wa Imani" (Muslim).
Nguvu zinatumika kwa yule aliye chini yako kama mtoto wako au watoto unaowalea na wengineo
Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala) Anasema: "Na kumbusha, kwani ukumbusho huwafaa Waumini" (51: 56). Na pia, "Na wao hawakutumwa wawe walinzi juu
Na tena: "Basi kumbusha! Hakika wewe ni Mkumbushaji. Wewe si mwenye kuwatawalia" (88: 21 – 22).
Tukumbuke pia kuwa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema:
"Miongoni mwa uzuri wa Uislamu wa mtu ni kuacha lisilomkhusu" (at-Tirmidhiy, nayo ni Hadiyth Hasan).
Nia yako na malengo ni mazuri
Na Allaah Anajua zaidi
- Login or register to post comments
- Email this page
- Chapisha


