Matunda Mchanganyiko Na Malai
Vipimo
Embe 3
Zabibu 2 vikombe
Stroberri 1 kikombe
Shammaam (tikiti cantelope) ½
Tikiti la asali (honey dew) ½
Tofaha (apples) 2
Peaches 3
Papayi ½
Juisi ya embe 2 vikombe
Malai (Cream) 1 kikombe
Namna Ya Kutayarisha
- Menya na katakata matunda yote isipokuwa zabibu utie katika bakuli
- Mimina juisi ya embe uchanganye vizuri
- Mwagia malai (cream) katikati au tia unapopakua katika vibakli vyake.
- Unaweza kulia pia na iskrimu (ice-cream) upendayo.
Kidokezo:
Unaweza kubadlisha matunda, kuongeza au kupungza upendavyo.
- Login or register to post comments
- Email this page
- Chapisha
