SW
Asaalam alaikum kwa mara nyengine tena ndugu zangu wa alhidaaya napenda kurejea suala langu tena kwenu. Kwamba je? Kusujudu wakati wa michezo hasa unapokuwa unashiriki katika michezo ikiwa wewe mwenyewe binafsi au mfano wako ukichukulia wakati huo tuseme unakua umevalia vifaa vya michezo ambavyo haviendani na sheria za kiislam labda umevaa kaptula fupi nk
JIBU:
Sifa zote njema Anastahiki Allaah Aliyetukuka Mola Mlezi wa walimwengu wote, Swalah na salamu zimshukie kipenzi chetu Mtume Muhammad (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) na Swahaba zake (Radhiya Allaahu ‘anhum) na watangu wema mpaka Siku ya Mwisho.
Shukrani zetu za dhati kwa swali lako kuhusu michezo, ushindi kwayo na kusujudu pindi unaposhinda.
Mwanzo tufahamu kuwa michezo mingi yenye kumpatia nguvu Muislamu imehimizwa
Kukubali huko ni kuifanyia istihzai Dini, na hakuna Muislamu mwenye Imani yake atakayekubali kufanya hivyo. Ikiwa ni hivyo mwana michezo huyo anaweza kufanya lolote atakalo baada ya kushinda. Lakini je, kufanya kwake huko kunakubaliwa kisheria? Jibu ni kuwa mtu huyo atakuwa anafanya makosa ya ziada baada ya kosa lake la kwanza. Na kufanya hivyo ni kuifanyia istihzai Dini yetu. Papo mahali pengi pa kufanyia sijdah kwa ajili ya Allaah Aliyetukuka hata kiwanjani lakini kwa jinsi hiyo haifai.
Tufahamu sijdah ya kushukuru ipo katika Dini yetu Tukufu lakini ni katika kheri inayokufikia wala sio katika michezo kama mpira au nyenginezo katika michezo tena katika hali ambayo Muislamu haifai kuwa kwayo, mathalan utakuta hayo ni mashindano ya kombe la pombe, au yanadhaminiwa na kampuni ya pombe, kamari, n.k.
Na Allaah Anajua zaidi