Sambusa Za Viazi

Vipimo
Viazi 4
Vitunguu nyasi vilokatwakatwa 3 miche
Kitunguu maji kilokatwakatwa 1
Chumvi 1 kijiko cha chai
Bizari ya pilau nzima ( jeera) 1 kijiko cha chai
Mafuta Nusu kilo
Manda za tayari 10 - 20
Yai 1 au 2
Namna Ya Kutayarisha Na Kupika
- Menya viazi, vioshe vikate slesi kisha vikatekate vipande vidogo vidogo.

- Chemsha maji kidogo ukiwa umeyatia chumvi , kisha vimimine viazi ndani ya maji yawache paka uwone tena yachemka kwa mara ya pili acha kwa dakika 10 - 15, kisha ondoa jikoni.
- Mimina katika chujio uchuje maji .
- Roweka bizari kwenye maji kwa muda wa dakika 20 hivi.
- Chukua bakuli kubwa lenye nafasi mimina viazi, vtunguu nyasi na maji, chumvi, mafuta vijiko 2 – 3 vya supu, na bizari. Changanya vizuri.
- Tandaza manda mezani au kwenye kibao fanya mkunjo wa sambusa kisha paka yai kwa brashi, kunja upate pembe moja . Tazama picha.

- Jaza viazi sehemu ulokunja kisha funga sambusa.

- Tia mafuta katika karai, yakipata moto, tia sambusa ziikaange hadi zigeuke rangi ya dhahabu.
- Zitoe na zichuje mafuta tayari kuliwa kwa Sosi Ya Ukwaju au Chatine Ya Mtindi Na Nanaa
- Login or register to post comments
- Chapisha
- Kutuma Kwa Email

asalaam alykum waramatullahi
asalaam alykum waramatullahi wabarakatu,
Niipi chatine ya nanaa?
Assalaam 'alayku Chatine ya
Assalaam 'alayku Chatine ya Nanaa imo katika kiungo kifuatacho
Saladi Na Sosi
na tumeshakuwekeeni tayari viungo katika upishi huu.
Jazaaka Allaahu Khayra