Tiba Gani Zimo Katika Qur-aan?

Tiba Gani Zimo Katika Qur-aan?

 

Alhidaaya.com

 

 

SWALI:

 

 

Kwanza: Sura gani ndani ya Quran ukiisoma, yaondosha mawazo ao stress?

Kisha naomba nifahamu dawa za Blood pressure (high or low) na ya kisukari zilizomo ndani ya Qurani. Nimepata kusikiya asali ni dawa, je yatibu nini?

 

 

JIBU:

 

AlhamduliLLaah Himidi Anastahiki Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa) Rabb wa walimwengu, Swalaah na salaam zimshukie Nabiy Muhammad (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) na Swahaba zake (Radhwiya Allaahu 'anhum) na waliowafuata kwa wema mpaka Siku ya Mwisho.

 

Hakuna Suwrah maalumu inayoondosha mawazo au dhiki bali Qur-aan nzima ni Shifaa (poza) ya magonjwa mbalimbali, Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

 

وَنُنَزِّلُ مِنَ الْقُرْآنِ مَا هُوَ شِفَاءٌ وَرَحْمَةٌ لِّلْمُؤْمِنِينَ ۙ وَلَا يَزِيدُ الظَّالِمِينَ إِلَّا خَسَارًا ﴿٨٢﴾

Na Tunateremsha katika Qur-aan ambayo ni shifaa na rahmah kwa Waumini; na wala haiwazidishii madhalimu isipokuwa khasara. [Al-Israa:82]

 

   قُلْ هُوَ لِلَّذِينَ آمَنُوا هُدًى وَشِفَاءٌ ۖ  

Sema: Hiyo ni kwa walioamini ni mwongozo na shifaa.  [Fuswilat:44]

 

Imaam As-Sa’dy (Rahimahu-Allaah) amesema: "Shifaa iliyokusanywa katika Qur-aan, kwa ujumla ni Shifaa ya moyo, na Shifaa ya mwili kutokana na maumivu yake na huzuni." [Tafsiyr As-Sa’diy] 

 

Na soma katika kiungo kifuatacho pia:

Imaam Ibn ‘Uthaymiyn: Qur-aan Ni Tiba Ya Maradhi Yaliyojaa Moyoni

 

Ama Suwratul-Faatihah imethibitika kwamba ni Shifaa ya magonjwa kama ilivyokuja katika Hadiyth ifuatayo:

 

عَنْ أَبِي سَعِيدٍ الْخُدْرِيِّ رضى الله عنه أَنَّ نَاسًا مِنْ أَصْحَابِ النَّبِيِّ صلى الله عليه وسلم أَتَوْا عَلَى حَىٍّ مِنْ أَحْيَاءِ الْعَرَبِ فَلَمْ يَقْرُوهُمْ، فَبَيْنَمَا هُمْ كَذَلِكَ إِذْ لُدِغَ سَيِّدُ أُولَئِكَ فَقَالُوا: هَلْ مَعَكُمْ مِنْ دَوَاءٍ أَوْ رَاقٍ؟ فَقَالُوا: إِنَّكُمْ لَمْ تَقْرُونَا، وَلاَ نَفْعَلُ حَتَّى تَجْعَلُوا لَنَا جُعْلاً‏.‏ فَجَعَلُوا لَهُمْ قَطِيعًا مِنَ الشَّاءِ، فَجَعَلَ يَقْرَأُ بِأُمِّ الْقُرْآنِ، وَيَجْمَعُ بُزَاقَهُ، وَيَتْفِلُ، فَبَرَأَ، فَأَتَوْا بِالشَّاءِ، فَقَالُوا: لاَ نَأْخُذُهُ حَتَّى نَسْأَلَ النَّبِيَّ صلى الله عليه وسلم فَسَأَلُوهُ، فَضَحِكَ وَقَالَ ‏:‏ ((وَمَا أَدْرَاكَ أَنَّهَا رُقْيَةٌ، خُذُوهَا، وَاضْرِبُوا لِي بِسَهْمٍ))

Abuu Sa’iyd Al-Khudriyy (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amehadithia kwamba: Baadhi ya Maswahaaba (wakiwa safarini) walifika karibu na kabila fulani la Waarabu, wakakataa kuwapokea. Walipobakia katika hali hiyo, huku mkuu wao alitafunwa na nyoka (au nge). Wakasema: Je, mna dawa yoyote au tabibu? Wakajibu: Nyinyi mmekataa kutupokea kwa hiyo hatutamtibu mgonjwa wenu hadi mtulipe! Wakakubali kuwapa kundi la kondoo. Mmoja wa Swahaaba akaanza kumsomea Suwratul-Faatihah huku akikusanya mate na kumtemea (mahali alipotafunwa). Mgonjwa akapona kisha watu wake wakawaletea kondoo lakini wakasema. Tusiwachukue mpaka tumuulize Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam). Walipomuuliza alicheka akasema: “Mmejuaje kuwa Suwratul-Faatihah ni ruqya? Wachukueni na nigaieni sehemu yangu.”  [Al-Bukhaariy]

 

Na Du’aa zifuatazo za Sunnah zinaondosha dhiki:

 

للّهُـمَّ إِنِّي عَبْـدُكَ، ابْنُ عَبْـدِكَ، ابْنُ أَمَتِـكَ نَاصِيَتِي بِيَـدِكَ، مَاضٍ فِيَّ حُكْمُكَ، عَدْلٌ فِيَّ قَضَاؤكَ، أَسْأَلُـكَ بِكُلِّ اسْمٍ هُوَ لَكَ، سَمَّـيْتَ بِهِ نَفْسَكَ، أِوْ أَنْزَلْتَـهُ فِي كِتَابِكَ، أَوْ عَلَّمْـتَهُ أَحَداً مِنْ خَلْقِـكَ، أَوِ اسْتَـأْثَرْتَ بِهِ فِي عِلْمِ الغَيْـبِ عِنْـدَكَ، أَنْ تَجْـعَلَ القُرْآنَ رَبِيـعَ قَلْبِـي، وَنورَ صَـدْرِي، وجَلَاءَ حُـزْنِي، وذَهَابَ هَمِّـي 

 

Ee Allaah hakika mimi ni mja Wako, mwana wa mja Wako, mwana wa mja wako mwanamke, utosi wangu uko Mikononi Mwako, yaliyopita kwangu yako katika hukumu Yako, ni usawa kwangu kunihukumu Kwako, nakuomba kwa kila Jina ambalo ni Lako Ulilojiita Kwako Mwenyewe au Uliloliteremsha katika Kitabu Chako, au Ulilomfundisha yoyote yule kati ya viumbe Vyako, au Ulilolihifadhi Wewe mwenyewe (na kujihusisha kulijuwa) katika ilimu ya ghaibu Kwako, nakuomba Ujaalie Qur-aan kuwa ni rabiy' (uhuisho, raha, furaha na ustawisho) wa moyo wangu na nuru ya kifua changu, na ufumbuzi wa  huzuni yangu [Hadiyth ya ‘Abdullaahi bin Mas-‘uwd (Radhwiya-Allaahu ‘anhu) - Ahmad (1/391) [452], Al-Haakim (1/509) na ameisahihisha Al-Albaaniy  (Rahimahu-Allaah) katika Al-Kalimi Atw-Twayyib [124].

 

Bonyeza viungo vifuatavyo upate du’aa hiyo kwa sauti pamoja na du’aa nyenginezo:

 

034-Hiswnul-Muslim: Du’aa Ukiwa Na Wahka Na Huzuni

041-Hiswnul-Muslim: Du’aa Ya Kulipa Deni, Kinga Ya Wahka, Huzuni, Uvivu, Ubakhili n.k

Swahiyh Twibbin-Nabawiy: Tiba Ya Nabiy Swalla Allaahu 'Alayhi Wa Aalihi Wa Sallam

 

Na pia majibu ya Swali katika kiungo kifuatacho:

 

Du’aa Zipi Kusoma Unapofikwa Na Shida, Dhiki Na Balaa?

 

Na kuhusu magonjwa na dawa zake, amesema Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) kwamba hakuna ugonjwa Aliouteremsha Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) isipokuwa Amejaalia pia kuweko na tiba yake:

 

عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رضى الله عنه عَنِ النَّبِيِّ صلى الله عليه وسلم قَالَ: ((مَا أَنْزَلَ اللَّهُ دَاءً إِلاَّ أَنْزَلَ لَهُ شِفَاءً)) رواه البخاري   

Imepokelewa kutoka kwa Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: ((Allaah Hakuteremsha maradhi isipokuwa Ameyateremshia shifaa)) [Al-Bukhaariy]

 

Ili kupata faida ziyada, bonyeza viungo vifuatavyo vilivyojaa mafunzo mbali mbali kuhusiana na tiba ya ki Shariy’ah ya kila aina ya maradhi:

Ruqyah: Kinga Na Tiba Katika Shariy'ah

Du’aa Za Ruqyah (Kinga) Faida Na Sharh Zake

 

Na dawa iliyo bora kabisa kutumia ni asali na habbat-sawdaa (mbegu nyeusi) kama ilivyotajwa katika Qur-aan na Sunnah: 

 

Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

 

 وَأَوْحَىٰ رَبُّكَ إِلَى النَّحْلِ أَنِ اتَّخِذِي مِنَ الْجِبَالِ بُيُوتًا وَمِنَ الشَّجَرِ وَمِمَّا يَعْرِشُونَ﴿٦٨﴾

Na Rabb wako Akamtia ilhamu nyuki kwamba: Jitengenezee nyumba katika majabali, na katika miti, na katika wanavyojenga.

 

ثُمَّ كُلِي مِن كُلِّ الثَّمَرَاتِ فَاسْلُكِي سُبُلَ رَبِّكِ ذُلُلًا ۚ يَخْرُجُ مِن بُطُونِهَا شَرَابٌ مُّخْتَلِفٌ أَلْوَانُهُ فِيهِ شِفَاءٌ لِّلنَّاسِ ۗ إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَآيَةً لِّقَوْمٍ يَتَفَكَّرُونَ﴿٦٩﴾

Kisha kula katika kila matunda, na fuata njia za Rabb wako zilizofanywa nyepesi (kuzipita). Kinatoka katika matumbo yao kinywaji cha rangi mbali mbali ndani yake mna shifaa (ya magonjwa) kwa watu. Hakika katika hayo, bila shaka ni Aayah (ishara, dalili) kwa watu wanaotafakari.   [An-Nahl:68-69] 

 

يقول رسول الله   صلى الله عليه وسلم  ((إن في الحبة السوداء شفاء من كل داء إلا السام))   اخرجه البخاري

Amesema Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam): “Katika habbat-sawdaa kuna shifaa (matibabu) ya kila maradhi isipokuwa mauti.” [Al-Bukhaariy]

 

Na Allaah Anajua zaidi

 

 

Share