Skip navigation.
Home kabah

Mitai-2

 

 

 

 

 

 

Vipimo

 

 

Unga wa ngano                                2 Magi (vikombe vikubwa)

 

Hamira                                            1 kijiko cha chai

 

Sukari                                              2 Vijiko vya supu

 

Maziwa                                            ¾ Magi

 

Siagi                                                2 Vijiko vya supu

 

Mafuta ya kukaangia                         Kiasi

 

 

 

 

Shira

 

 

Sukari                                       ¾ Magi

 

Maji                                          ¾ Magi

 

Illiki ya unga                             Kiasi

 

Zafarani                                   Kiasi

 

 

 

 

Namna Ya Kutayarisha Na Kupika

 

 

 

  1. Katika bakuli, changanya vipimo vyote pamoja na ukande unga usiwe mgumu wala laini sana uwe kiasi.
  2. Kisha fanya donge moja na iache pahali penye joto mpaka iimuke.
  3. Halafu weka mafuta ya kukaangia kwenye moto.
  4. Sukuma donge hadi liwe duara sio nyembamba sana, kisha katakata kama ilivyo kwenye picha.
  5. Mafuta ya kisha pata moto choma mittai hukuunazigeuza hadi ziwive na kugeuka rangi.
  6. Katika sufuria tia vipimo vya shira na iache ichemke isiwe nzito sana.
  7. Mimina mitai kwenye shira na uzipepete, kisha weka kwenye sahani na zitakuwa tayari kwa kuliwa.