Umetanguliza Nini Aakhirah Ee Ndugu Muislamu?

Umetanguliza Nini Aakhirah Ee Ndugu Muislam?

 

Alhidaaya.com

 

 

 

Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta’alaa):

 

يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا اتَّقُوا اللَّـهَ وَلْتَنظُرْ نَفْسٌ مَّا قَدَّمَتْ لِغَدٍ ۖ وَاتَّقُوا اللَّـهَ ۚ إِنَّ اللَّـهَ خَبِيرٌ بِمَا تَعْمَلُونَ﴿١٨﴾

“Enyi walioamini! Mcheni Allaah, na nafsi itazame imetanguliza nini kwa ajili ya kesho, na mcheni Allaah. Hakika Allaah ni Mwenye upeo wa khabari za dhahiri na za kufichika kwa yale myatendayo.” [Al-Hashr: 18]

 

Siku ya Qiyaamah katika Qur-aan imetajwa kwa majina kadhaa. Baadhi ya ‘Ulamaa wamenukuu idadi yake kuwa ni majina thelathini na moja takriban. Miongoni mwayo; Al-Ghad  (kesho),  As-Saa'ah (saa), At-Taghaabun (siku ya hasara au siku ya kulipizana), Yawmul-Ba'th (siku ya kufufuliwa), Yawmul-Aakhirah (siku ya Mwisho), Yawmud-Diyn (siku ya malipo), Yawmul-Faswl (siku ya hukumu), Al-Waaqi'ah (tukio), Yawmul-Wa'iyd (siku ya makamio) na kadhalika.

 

Aayah hiyo imetajwa pia katika Hadiyth ifuatayo:

 

عَنْ جَرِيرِ بْنِ عَبْدِ اللَّهِ (رضي الله عنه) قَالَ:  كُنَّا عِنْدَ رَسُولِ اللَّهِ (صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ) فِي صَدْرِ النَّهَارِ فَجَاءَ قَوْمٌ عُرَاةً حُفَاةً مُتَقَلِّدِي السُّيُوفِ عَامَّتُهُمْ مِنْ مُضَرَ ، بَلْ كُلُّهُمْ مِنْ مُضَرَ ، فَتَغَيَّرَ وَجْهُ رَسُولِ اللَّهِ (صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ) لِمَا رَأَى بِهِمْ مِنْ الْفَاقَةِ ، فَدَخَلَ ثُمَّ خَرَجَ.  فَأَمَرَ بِلاَلاً فَأَذَّنَ فَأَقَامَ الصّلاَةَ فَصَلَّى ثُمَّ خَطَبَ فَقَالَ:  يَا أَيُّهَا النَّاسُ اتَّقُوا رَبَّكُمُ الَّذِي خَلَقَكُم مِّن نَّفْسٍ وَاحِدَةٍ وَخَلَقَ مِنْهَا زَوْجَهَا وَبَثَّ مِنْهُمَا رِجَالًا كَثِيرًا وَنِسَاءً ۚ وَاتَّقُوا اللَّـهَ الَّذِي تَسَاءَلُونَ بِهِ وَالْأَرْحَامَ ۚ إِنَّ اللَّـهَ كَانَ عَلَيْكُمْ رَقِيبًا ﴿١﴾ و اتَّقُوا اللَّـهَ وَلْتَنظُرْ نَفْسٌ مَّا قَدَّمَتْ لِغَدٍ ۖ   تَصَدَّقَ رَجُلٌ مِنْ دِينَارِهِ مِنْ دِرْهَمِهِ مِنْ ثَوْبِهِ مِنْ صَاعِ بُرِّهِ مِنْ صَاعِ تَمْرِهِ وَلَوْ بِشِقِّ تَمْرَةٍ ، فَجَاءَ رَجُلٌ مِنْ الأَنْصَارِ بِصُرَّةٍ كَادَتْ كَفُّهُ تَعْجِزُ عَنْهَا ، بَلْ قَدْ عَجَزَتْ ، ثُمَّ تَتَابَعَ النَّاسُ حَتَّى رَأَيْتُ كَوْمَيْنِ مِنْ طَعَامٍ وَثِيَابٍ حَتَّى رَأَيْتُ وَجْهَ رَسُولِ اللَّهِ (صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ) يَتَهَلَّلُ كَأَنَّهُ مُذْهَبَةٌ. فَقَالَ رَسُولُ اللَّهِ (صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّم)َ:  ((مَنْ سَنَّ فِي الإِسلاَمِ سُنَّةً حَسَنَةً فَلَهُ أَجْرُهَا وَأَجْرُ مَنْ عَمِلَ بِهَا مِنْ غَيْرِ أَنْ يَنْقُصَ مِنْ أُجُورِهِمْ شَيْئًا ، وَمَنْ سَنَّ فِي الإِسلاَمِ  سُنَّةً سَيِّئَةً فَعَلَيْهِ وِزْرُهَا وَوِزْرُ مَنْ عَمِلَ بِهَا مِنْ غَيْرِ أَنْ يَنْقُصَ مِنْ أَوْزَارِهِمْ شَيْئًا))

 

Imepokelewa kutoka kwa Jariyr  bin ‘Abdillaah (Radhwiya Allaahu ‘anhu) ambaye amesema : “Tulikuwa na Rasuli wa Allaah Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam mapema mchana, wakaja watu ambao walikaribia kuwa [kwa mavazi yao ya duni], hawana viatu wakiwa wemebeba mapanga yao. Wengi wao ikiwa si wote walikuwa kutoka (kabila la) Mudhwar. Uso wa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) ukabadilika alipoona hali waliyonayo ya umasikini. (akawa amehuzunika). Akaingia (nyumbani kwake) kisha akatoka nje na akamuamrisha Bilaal aadhini. Akaswalisha watu kisha akahutubia akisema:

 

يَا أَيُّهَا النَّاسُ اتَّقُوا رَبَّكُمُ الَّذِي خَلَقَكُم مِّن نَّفْسٍ وَاحِدَةٍ وَخَلَقَ مِنْهَا زَوْجَهَا وَبَثَّ مِنْهُمَا رِجَالًا كَثِيرًا وَنِسَاءً ۚ وَاتَّقُوا اللَّـهَ الَّذِي تَسَاءَلُونَ بِهِ وَالْأَرْحَامَ ۚ إِنَّ اللَّـهَ كَانَ عَلَيْكُمْ رَقِيبًا ﴿١﴾ و اتَّقُوا اللَّـهَ وَلْتَنظُرْ نَفْسٌ مَّا قَدَّمَتْ لِغَدٍ ۖ

 

“Enyi watu! Mcheni Rabb wenu Ambaye Amekuumbeni kutokana na nafsi moja (Aadam) na Akaumba kutoka humo mke wake (Hawwaa) na Akaeneza kutoka hao wawili wanaume na wanawake wengi. Na mcheni Allaah Ambaye Kwake mnaombana (haki zenu kwa kuunga) undugu. Hakika Allaah ni Mwenye kuwachunga daima. [An-Nisaa: 1]. Na Mcheni Allaah, na nafsi itazame imetanguliza nini kwa ajili ya kesho (Siku ya Qiyaamah”. [Al-Hashr: 18].  “Atoe mtu sadaka katika dinari zake, nguo zake, ngano au tende zake hata ikiwa ni nusu tende.” Akaja mtu kutoka Answaar akaleta furushi ambalo hakuweza hata kulibeba vizuri mkononi, kisha mwengine, kisha mwengine hadi yakawa marundi mawili ya chakula na nguo. Nikaona uso wa Rasuli wa Allaah Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam ukinawiri kwa furaha. Akasema Rasuli wa Allaah Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam: “Atakayeanza (kutenda) katika Uislaam kitendo chema, atapata thawabu zake na thawabu sawasawa na watakaomfuata bila ya kupunguziwa chochote katika thawabu zao. Na atakayeanzisha (kutenda) kitendo kiovu atabeba dhambi zake na dhambi za watakaomfuata bila ya kupungiziwa katika dhambi zao chochote)) [Muslim ameisimulia Hadiyth hii kutokana na isnaad ya Shu'bah]   

                          

Kwa hayo, jiulize Muislamu, je, umetanguliza nini Aakhirah? Umetimiza Swalaah zako ipasavyo? Umetanguliza Swalaah za Sunnah?  Umetekeleza Zakaah na umetoa swadaqah? Umefunga Swiyaam za Ramadhwaan na Swiyaam za Sunnah? Umetekeleza Hajj na 'Umrah? Umesoma Qur-aan kwa wingi na kufuata maamrisho yake na kujiepusha na makatazo yake?  Umeamrisha mema na kukataza maovu? Umetanguliza wema wa aina yoyote?

 

Kumbuka kwamba jema lolote utakalolitenda litakuwa ni akiba yako Aakhirah na bila shaka utakuja kulikuta na utapata  malipo yake siku ya Qiyaamah kama

Anavyosema Allaah (Subhaanau wa Ta’alaa):

 

وَأَقِيمُوا الصَّلَاةَ وَآتُوا الزَّكَاةَ ۚ وَمَا تُقَدِّمُوا لِأَنفُسِكُم مِّنْ خَيْرٍ تَجِدُوهُ عِندَ اللَّـهِ ۗ إِنَّ اللَّـهَ بِمَا تَعْمَلُونَ بَصِيرٌ ﴿١١٠﴾

“Na simamisheni Swalaah na toeni Zakaah, na lolote mnalolitanguliza kwa ajili ya nafsi zenu katika khayr mtalikuta kwa Allaah, hakika Allaah kwa yale myafanyao ni Mwenye kuona.” [Al-Baqarah: 110]

 

 

Share