Mke Baada Ya Kuachika Kaingia Katika Maasi Ya Zinaa, Na Nini Hukmu Ya Mawasiliano Kwa Walioachana?

SWALI

 

A. aleykum nafurahi sana na majibu yenu ila nilikua nataka kuuliza
ikiwa mke na mume wameachana na wamezaa watoto lakini yule mwanamke baada ya kuachana na mume akajiingiza kwenye ukahaba nini hukum yake? Na ni halali kuwasliana na mume alieachana nae kwa njia ya simu?


 

 

JIBU:

 

Sifa zote njema Anastahiki Allaah Aliyetukuka Mola Mlezi wa walimwengu wote, Swalah na salamu zimshukie kipenzi chetu Mtume Muhammad (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) na Swahaba zake (Radhiya Allaahu ‘anhum) na watangu wema mpaka Siku ya Mwisho.

 

 

Shukrani zetu kwa swali lako kuhusu mke kuingia katika maasiya baada ya kuachwa, na mawasiliano baina ya walioachana.

Hakika mwanamke kuingia kwenye zinaa baada ya kuachwa ni dhambi kubwa. Kama kungekuwa na shar’iah ya Kiislamu yenye kutawala leo hii basi hukmu yake ni kuuliwa.

 

Hata hivyo, la kufanywa wakati huu ni kutafutwa njia muafaka za kumshauri na kumnasihi aache maasiya hayo kwani ni dhambi kubwa kwake. Na kufanyika hilo kunaweza kutumiwa njia mbali mbali kama vile kutumiwa wazazi wake, jamaa zake, wanavyuoni wa Kiislamu na njia nyenginezo.

 

Ama mume na mke walioachana wanaweza kuwasiliana kwa simu kwa dharura ima kuhusiana na maslahi ya watoto wao na mfano wa hayo yanayokubalika kishari’ah. Ama mawasiliano ya wao kusalimiana na kukumbushana ya nyuma, hayo ni mambo yasiyofaa kwani yanapelekea kuleta fitna na kukurubia zinaa.

 

Na Allaah Anajua zaidi

 

 

Share