Fadhila Za Hajj Na 'Umrah Na Adabu Zake
Ukht Muznah Faraj
Alhamdulillahi Rabbil Alaamiyn Was swalatu Wassalaamu Alaa Nabiyyinaa Waalaa Aalihi Waswahbihi Waman Tabiahum bi’ihsaani ilaa yaumid’diyn. Amma Ba’ad,
1- Amesema Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala)
((Walillahi Alla Nnasi Hijjul Bayti Manistata’a Ilayhi Sabiyla, Waman kafara Fainna llaha Ghaniyun anil Aalamiin.))
((Na Mwenyeezi Mungu amewawajibishia watu wafanye hajji katika nyumba hiyo; (Al-Ka’abah) Yule awezae kufunga safari kwenda huko. Na atakae kanusha (asende, hali kuwa anaweza) basi Mwenyeezi Mungu simuhitaji kuwahitajia walimwengu))
“Qur’aan: 3:97”
2- Na amesema Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) : ((Al-'Umrata ilal 'Umrah kaffaaratul limaa baynahuma, wal-Hajjul-Mabruur laysa lahuu jaza’a illal jannah))
((Kufanya umrah hadi umrah hufutiwa madhambi baina yake, na Hajj (Mabruur) yenye kukubaliwa haina malipo isipokuwa pepo))
{Imepokewa na Al-Bukhaariy na Muslim}
3- Na amesema Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) : ((Man hajjah falam yarfuth walam yafsuq raja’a min dhunubihi
((Atakayehiji ikawa hakufanya maovu (kwa vitendo wala kwa maneno) na wala hakuvunja amri za Allaah (Subhaanahu Wata’ala) atasamehewa madhambi yake yote atakuwa
{Imepokewa na Al-Bukhaariy na Muslim}
4- ((Na amesema Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) :(Khudhuu anniy manasikakum)).
((Chukueni Hajj kutoka kwangu))
{Imepokewa na Muslim}
5- Ni wajibu wa kila mwenye kuhiji na kufanya umrah awe
((InnAllaaha taala twayyibun laa yaqbalu illaa twayyiba))
((Hakika Mwenyeezi Mungu Mtukufu ni mzuri na hakubali isipokawa kizuri))
{Imepokewa na Muslim}
6- Kwa hakika hajji ni kongamano kubwa kwa waislamu linalo wakutanisha waislamu, kwa sababu kunapatikana ndani yake kujuana, kupendana, na kusaidiana katika kutatua matatizo juu ya kila hali, na pia kushuhudia manufaa yanayopatikana humo ya dini na dunia. SubhaanAllaah!!! Ametukuka Aliye Mbora wa viumbe.
Na Amesema Allaah Mtukufu:
((Wata'awanuu alal birri wat taqwaa wala ta'awanuu 'alal ithmi wal uduwaan))
((Na saidianeni kwa wema na ucha Mungu wala msisaidaene katika madhambi na uadui))
“Qur’aan: 5:2
7- Inajuzu kufanya umrah katika wakati wowote, lakini kufanya umrah katika mwezi wa Ramadhaan ni bora, kwa kauli aliyosema Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam)
(('Umrah fiy Ramadhaan tu’adilu Hajjah))
((Kufanya 'Umrah katika mwezi wa Ramadhaan ni
{Al-Bukhaariy na Muslim}
8- Swalah katika msikiti mtukufu wa Makkah ni bora mara laki moja kuliko swala katika Misikiti mingine. Kwa kauli aliyosema Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam):
((Swalaatu fiy masjidiy hadhaa afdhalu min alfi swalati fiymaa siwaahu minal masaajid illa Masjidil Ka’abah))
((Swalah katika msikiti wangu huu ni bora katika Swalah elfu moja kuliko misikiti mingine iispokuwa Msikiti mtukufu wa Makkah)) (Imepokewa na Muslim)
Swala moja katika msikiti wa Mtume madina ni sawa malipo yake na Swalah elfu moja. (1000)
Na amesema Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) :
((was swalaatu fiyl masjidil haraam afdhalu min swalaati fiy masjidiy hadhaa bimiati swalaati))
((Swalah katika Msikiti mtukufu wa Makkah ni bora kuliko Swalah katika msikiti wangu huu kwa Swalah mia))
(Imepokewa na Ahmad)
Akimaanisha mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) kuwa swala moja ni sawa na swala mia, yaani 100*1000 = 100,000 .
Hii ni kuonyesha kuna fadhila kubwa
KWA UFUPI:
Hajji ni nguzo miongoni mwa nguzo za kiislamu na ndani yake kuna fadhila nyingi ambazo nimezitaja kwa ufupi na manufaa ya kidunia na akhera. Kwa mfano unaweza kufanya biashara pindi umalizapo hajji na mengineyo ambayo tuliyataja hapo juu. Na manufaa ya akhera ambayo ni bora zaidi kuliko ya dunia.
Allaah amesema:
(( Walal aakhiratu khayrun wa abqaa))
((Na maisha ( bora zaidi kabisa ) ni ya akhera yenye kudumu))
“Qur-aan: 87:17”
Basi ni juu ya kila muislamu ajitahidi kuendea njia hiyo pale atapo kuwa na uwezo wa kuifikia njia hiyo kabla hayajamfikia mauti hali yuko katika maaswi. Basi na ajihadhari kutokana na maovu, kuvunja amri za Allaah, mijadala isiyo ya hakki wala faida ndani yake na maaswi yote kwa ujumla.
ADABU ZA HAJJ NA UMRAH:
1- Itakase hajji yako iwe kwa ajili ya Allaah (Subhaanahu Wata’ala) na sema
kama alivyosema Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam)
((Allaahumma hajjatan laa riyaa’a fiyhaa walaa sum’ah))
((Ewe Mola (mtukufu) ifanye Hajj yangu isiwe ya kujionyesha wala kusifiwa))
{Swahiyh Al-Bayhaqiy}
Kwani kuna baadhi ya watu matendo yao wanayafanya ili waonekane na wao wamekwenda au wamefanya hajji au wamesikilikana kwa kusifiwa kama Fulani pia amekwenda iwe ni matendo ya hajji au hata ibada zozote ilihali si kwa ajili ya Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala) hao matendo yao yatakuwa hayana malipo yoyote mbele ya Mwenyeezi Mungu Mtukufu.
2- Iwe hajji imewafikiana na hajji aliohijji Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam)
Amesema :(( khudhuu anniy manaasika kum) )
((Chukueni Hajj kutoka kwangu))
{imepokewa na Muslim}
3- Jihadhari na kutokufanya maovu na yaliyo katazwa, na maaswi, na mijadala iliyo baatili (iliyokatazwa) mpaka hijjah yako iwe ni maqbuul ( yenye kukubalika).
4- Jihadhari na kuomba duaa kwa asie kuwa Mwenyeezi Mungu Mtukufu. kuomba maiti mfano kwenye makaburi wakati unapo zuru makaburi ni kwa ajili ya kujikumbusha na mauti na kuwatakia rehma na maghfira sikuwaomba au kutaka msaada au kuokolewa hiyo itakuwa ni shirki ambayo itabatilisha hajji na amali zako zote.
((lain ashrakta layahbatwanna amaluka walaa takunanna minal khasiriyn))
((Ikiwa utamshirikisha (Mwenyeezi Mungu ) bila shaka matendo yako yote yataruka patupu (hutazipatia thawabu japo ni matendo mazuri ) na lazima utakuwa miongoni mwa wenye khasara))
“Qur-aan 39:65”
5- Unatakiwa uwe mpole kwa walio karibu yako yaani walioko pembezoni mwako wakati unapokuwa unafanya twawafu (kuizunguka al ka’abah) na unapo fanya saa’yi (kutembea kilima cha saffa na mar’wah) na wakati wa kutupa mawe katika minara ya jamaraati, wala msinyanyuwe sauti wakati wa kumtaja Mwenyeezi Mungu wala wakati wa Duaa na khasa pale mnapokuwa kwenye kundi kwani kunyanyuwa sauti kunawachanganya wengine kwakufanya hivyo hakuna dalili na hivyo kunyanyuwa sauti ni Bid’aa iliyozushwa.
6- Haifai kufanya zahma yaani kusukumana wakati wa kuliendea jiwe jeusi wala kusimama hapo kuwazulia wengine wakati unapo fanya tawaafu. Inavotakiwa ni kuligusa, kulibusu na huku unaomba nakuondoka si kusukumana.
7- Kusimama wakati wa Sa’yi kati ya Swaffa na Marwah pindi inapo nadiwa swala ya Jama'ah mpaka itapomalizika Swalah utatimiza palipobaki.
8- Kuhifadhi Swalah ya Jama'ah katika msikiti na khasa unapokuwa katika Msikiti wa Makkah, Kwani kuna fadhila kubwa
9- Usiwapitepite wenye kuswali ukawaudhi, kaa palipo karibu yako penye nafasi.
10- Jihadhari na kuwapita watu wanapo kuwa kwenye safu ya Swalah kati yako na mwenye kuswali hata kama ni katika msikiti mtukufu wa Makkah ili upite safu ya mbele ikiwa unataka kukaa mbele basi inakubidi uwahi na sio kuwakunja watu shingo ili upite mbele, kwani hayo ni matendo ya shaitwani, isipokuwa iwe kwa dharura.
11- Kuzidisha kuizunguka al ka’abah kwani kufanya hivyo kuna malipo makubwa kama alivyo sema Mtume
(Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam)
((man twaafa bil bayti sab’an, wa swalla rakaatein, kaana kaatiki raqabah))
((Mwenye kuizunguka Al-Ka’abah mara saba atakuwa
{Imepokewa na Ibn Maajah}
12- Haifai kuchinja kabla ya kufikia siku ya kuchinja wala haifai kutoa sadaka kwa thamani yake.
13- Na katika alama za kukubaliwa hajji ni kubadilika katika hali iliyo nzuri ya aqidah yako (kutokumshirikisha Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala) katika ibaada zako kushirikiana na Waislamu wenzio kwa wema na tabia njema na ni juu yako kumuomba Mwenyeezi Mungu wakati wote hii ni kipimo baada ya hajji kwani ikiwa hukubadilika katika 'Aqidah yako na tabia yako kwa ujumla itakuwa hajji yako ni matembezi tu na sio (Mabruur)
((Rabbanaa taqabbal minnaa innaka antas samiul aliym))
((Ewe Mola Tukubalie hakika Wewe ni Mwenye kusikia na ni mjuzi))
“Aamiyn”
Allaah Atuwafiqishe na Atufanyie wepesi na ajaalie manufaa na kuyafanyia kazi yote na tufaidike nayo InshaAllaah.
WAllaahu A’alam
- Login or register to post comments
- Email this page
- Chapisha


