Vikeki Vidogo Vya Mviringo (Muffins) Vya Tende Na Lozi

Vikeki Vidogo Vya Mviringo (Muffins) Vya Tende Na Lozi

 

Vipimo: 

Unga -  2 ½ vikombe

Sukari - 1 kikombe

Chumvi - 1 kijiko cha chai

Mdalasini wa unga -  1 kijiko cha chai

Baking Powder - 3 vijiko vya chai

Vanilla - 1 kijiko cha chai

Mayai -  3

Siagi laini -  350 gm

Maziwa mazito (condensed milk) - 1 kikopo

Maziwa ya maji - 1 ½ kikombe

Tende iliyokatwakatwa - 1 ½ kikombe

Lozi zilizomenywa na kukatwakatwa slesi -  ½ kikombe 

Namna Ya Kutayarisha Na Kupika 

  1. Katika bakuli, changanya vitu vikavu vyote (unga, sukari, chumvi, mdalasini, baking powder).
  2. Tia katika bakuli jengine, mayai, siagi, maziwa mazito (condensed), maziwa ya maji, vanilla, na uchanganye vizuri.
  3. Changanya michanganyiko miwili hiyo pamoja.
  4. Changanya na tende iliyokatwa katwa .
  5. Mimina mchanganyiko katika vibati vya kupikia keki au karatasi za cup cakes.
  6. Nyunyizia  lozi kisha uchome (Bake) katika moto wa 350°- 450°  kwa muda wa nusu saa uhakikishe zimewiva.
  7. Epua zikiwa tayari kuliwa.

Kidokezo:

Unaweza kufanya nusu za lozi pekee

Unaweza kutia chokoleti badala ya tende

 

 

Share