Keki Ya Machungwa

 Keki Ya Machungwa

Vipimo 

Siagi iliyolainika -  ½ Kikombe cha chai

Sukari -  1 Kikombe cha chai

Mayai -  2

Maganda ya chungwa  iliyokwaruzwa - 1 Kijiko cha supu 

Ariki ya lozi (almond essence) -  ¼  Kijiko cha chai

Unga - 2 Vikombe vya chai

Baking powder -  2 Vijiko cha chai

Chumvi -  ½ Kijiko cha chai

Iliki ya unga -  ½  Kijiko cha chai

Maziwa -  ½ Kikombe cha chai

Juisi ya machungwa -  ¼  Kikombe cha chai

Lozi ziliyokaangwa na kupondwa -  ¾  Kikombe cha chai

 

Namna Ya Kutayarisha Na Kupika

  1. Washa oveni moto wa 350ºF.
  2. Paka siagi chombo utakachochomea (ikiwa unatumia loaf pan ndogo, utahitaji 3)
  3. Katika bakuli la mashine, saga sukari na siagi hadi ilainike.
  4. Kisha tia yai moja moja, halafu ganda la chungwa na ariki ya lozi.
  5. Katika bakuli jengine, changanya pamoja unga, baking powder, chumvi na iliki.
  6. Kisha changanya kwenye ule mchanganyiko wa siagi, halafu tia maziwa na juisi ya machungwa, na lozi.
  7. Vumbika kwenye oveni kwa muda wa dakika 35.
  8. Iache ipowe kabisa na itakuwa tayari kuliwa. 

 

 

Share