Viazi Vya Jibini Na Maziwa
Viazi Vya Jibini Na Maziwa

Vipimo
Viazi- 7-9
Maziwa ya kopo(evaporated milk) - 1 mkebe
Unga wa ngano - ½ kikombe cha chai
Siagi - 4 vijiko vya chakula
Chumvi - kiasi
Namna Yakutayarisha
- Anza kuwasha oveni moto wa 350°F.
 - vioshe viazi vizuri na maganda yake kisha kata slesi za duara.
 - halafu pakaza siagi kwenye treya ya kuchomea na panga slesi za viazi zikiwa zinakaliana juu ya slesi nyingine.
 - kisha mimina maziwa ya kopo kiasi kuziba ziba kila kiazi.
 - Kisha nyunyizia chumvi na nyunyizia na unga kijiko kimoja halafu dondoshea siagi au butter matone matone kwenye treya yote juu ya viazi.
 - kisha panga tena viazi juu yake kama ulivyofanya mwanzo, tia chumvi, unga na matone ya mafuta mpaka treya ijae.
 - Halafu malizia juu kumimina maziwa yote yaliyobaki.
 - kwa ladha nzuri badala ya maziwa ya kopo ni bora kunyunyizia urojo wa bashameli.(tazama kwenye macaroni ya bashameli kupata vipimo na kutayarisha bashameli)
 - mwisho tia kwenye oven kwa muda wa dakika 30-45 au mpaka viazi viwive vizuri. Epua na tayari kwa kuliwa.
 
    
    