Ndoa Ya Waliofanya Zinaa
SWALI
Asalaam Alaikum Warahmatulhaahi Wabarakaatuhu, mimi sijambo [ Al Hamdulillaah] kama nanyi hamjambo viongozi wetu wa Dini ya kweli basi ni kheri. Naomba msaada mnijibu
Walioanza kufanya zinaa kabla ya ndoa, wakitaka kuoana wanaruhusiwa?
JIBU:
Shukrani zote anastahiki Allah, Mola Mlezi wa viumbe vyote. Pia shukrani ni kwa ndugu zetu kwa kaka na dada zetu wanaouliza maswali na kaka yetu huyu ambaye ameuliza haya maswali takriban tisa
Watu hao wawili wanaruhusiwa kuoana baada ya kukamilisha masharti Fulani. Sharti muhimu sana ni kujuta kwa kitendo hicho na kuomba msamaha kwa kufanya hivyo na azimie kutorudia tena, na lau kungekuwa na dola ya Kiislamu basi angejipeleka ili ahukumiwe, na pia kufanya mambo mazuri kwani Mtume s.a.w.w. amesema: “Mche Allah popote pale ulipo. Na fuatisha baya kwa zuri nalo litalifuta
Na baada ya kufanya hivyo hawatakiwi kukaa pamoja na wale wasifanye kitendo hicho mara nyingine. Wanatakiwa wawe mbali kwa muda wa miezi mitatu ili kuhakikisha
“Mzinifu haolewi ila na mwanamume mzinifu au mshirikina. Na hayo ya. Mwanamume mzinifu hamwoi ila mwanamke mzinifu au mwanamke mshirikina. Na mwanamke meharimishwa kwa Waumini” (24: 3).
Tanbihi: Uislamu umefanya ndoa kuwa ni nyepesi kutekelezeka hivyo ni kwa vijana na wasichana wasijipeleke katika mambo ambayo yanaleta matamanio badala yake waoane na hili linapunguza mengi na pia kujiondoa na mengi yaliyo machafu na ya uasherati. Na Mtume ametupatia kinga pale alipowahutubia vijana: “Enyi kongamano la vijana! Yule mwenye uwezo wa kuoa na afanye hivyo, kwani
Kwa maelezo zaidi, tafadhali soma majibu yalioko katika viungo vifuatavyo:
WAZINIFU WALIOTUBU WANAWEA KUFANYA NDOA NA WALIOTAKASIKA?
Wa Allaahu A'alam
- Login or register to post comments
- Email this page
- Chapisha


