Ukumbusho Wa Kuzuia Kukata Kucha Na Nywele Kwa Anayenuia Kuchinja

Ukumbusho Wa Kuzuia Kukata Kucha Na Nywele Kwa Anayetaka Kuchinja

 

 

Alhidaaya.com

 

 

Tunapenda kuwakumbusha ndugu zetu wengi jambo ambalo wanaghafilika nalo, kuwa, wenye kunuia kuchinja au kuchinjiwa (anayewakilisha mtu kumchinjia), kuanzia unapoandama tu mwezi wa Dhul-Hijjah wanatakiwa wajizuie kukata nywele za mwili na kukata kucha mpaka watakapomaliza kuchinja. Haya ni maamrisho yanayopatikana katika Hadiyth ifuatayo:  

 

عن أم سلمة رضي الله عنها أن النبي صلى الله عليه وسلم قال: ((إِذَا رَأَيْتُمْ هِلَالَ ذِي الْحِجَّةِ وَأَرَادَ أَحَدُكُمْ أَنْ يُضَحِّيَ ، فَلْيُمْسِكْ عَنْ شَعْرِهِ وَأَظْفَارِهِ )) وفي رواية: ((فَلا يَمَسَّ مِنْ شَعَرِهِ وَبَشَرِهِ شَيْئًا))

Ummu Salamah (Radhwiya Allaahu 'anhaa) amehadithia kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: ((Ukiandama mwezi wa Dhul-Hijjah na ikiwa yuko anayetaka kuchinja basi azuie (asikate) nywele zake na kucha zake)) na katika riwaaya nyengine ya Muslim (1977); ((basi asitoe kitu katika nywele zake wala ngozi yake)) [Muslim]

 

Faida na mafunzo ziyada yafuatayo:

 

Kuchinja - Fadhila, Hikmah Na Hukmu Zake

Al-Lajnah Ad-Daaimah: Anayetia Niyyah Kuchinja Asikate Au Kunyoa Nywele Au Kukata Kucha

 

 

Al-Lajnah Ad-Daaimah: Nani Wa Kujizuia Kukata Nywele Na Kucha Katika Kuchinja (Udhwhiyah)?

 

 

Imaam Ibn 'Uthaymiyn: Udhwhiyah (Kuchinja) Ni Sunnah Iliyosisitizwa Kwa Mwenye Uwezo

 

 

Imaam Ibn Baaz - Vipi Kuigawa Nyama Ya Udhw-hiyah

 

 

Imaam Ibn ‘Uthaymiyn: Kuigawa Nyama Ya Udhw-hiyah Kama Zawadi Au Swadaqah Iwe Freshi Si Ya Kupikwa

 

 

Imaam Ibn 'Uthaymiyn: Masharti Ya Udhwhiyah Ni Yepi?

 

 

Imaam Ibn 'Uthaymiyn: Haijuzu Kumpa Mchinjaji Wa Udhw-hiyah Nyama Kama Ujira Wake

 

 

 

Imaam Ibn Baaz - Hukmu Ya Kuchinja Kwa Kutumia Mkono Wa Kushoto

 

 

Kuzuia Kukata Nywele Na Kukata Kucha Ni Kwa Familia Nzima Au Kwa Mtu Mmoja Anayechinja Au Kugharamia Uchinjaji?

 

 

 

 

 

Share