Keki Ya Tende Kwa Karameli Ya Tangawizi

Keki Ya Tende Kwa Karameli Ya Tangawizi

 

Vipimo

 

Unga -  3 kikombe

Baking powder  -  3 Vijiko vya chai

Sukari  -  ½ Kikombe

Tende iliyokatwa ndogo ndogo - 2 vikombe

Maji yamoto -  2 vikombe

Siagi - 4 Vijiko vya supu (au vikombe 2 vya kahawa)

Mayai - 2

Cream -  300 gm (au vikombe 2 Vya Kahawa)

Tangawizi ya powder -   1 kijiko cha

Mdalasini - 1  kijiko cha chai

Hiliki -   ½  kijiko cha chai

Vanilla - 4  vijiko vya chai 

 

Vipimo Vya Karamel 

 

Sukari ya buni (brown sugar) -  5 Vijiko vya supu

Siagi -  6 Vijiko vya supu

Tangawizi ya powder - 1 kijiko cha chai

 

Namna Ya Kutayarisha Na Kupika 

  1. Tia maji ya moto katika tende kuiroweka kidogo.
  2. Changanya unga na baking powder vizuri katika bakuli.
  3. Tia vitu vyote vingine na uchanganye vizuri.
  4. Mimina katika bati la duara la kupikia keki ulilolipaka siagi kidogo la kiasi ya 10 in dia x 2 in    
  5. Ipikie (bake) katika moto  wa 300° kwa muda wa kama ¾  saa au zaidi hadi iwive.
  6. Iweke katika sahani au bakuli la keki na mwagia karamel juu yake.

 

Namna Ya Kutayarisha Karamel

 

Yayusha siagi katika sufuria ndogo au frying pan kisha tia sukari ya brown.

Tia tangawizi changanya.

Inapoyayuka, mwagia katika keki

 

 

Bis-swihhah wal-hanaa (kula kwa siha na kuburudika)

 

 

 

Share