Skip navigation.
Home kabah

Bajia Za Kunde

VIPIMO

 

Kunde                                                                     1 ½  Vikombe

 
Vitungu vya kijani iliyokatwa katwa                       ½  Kikombe

 
Baking soda                                                            ¼  Kijiko cha chai

 
Masala                                                                    1  Kijiko cha chai

 
Maziwa                                                                   2 Vijiko vya supu

 
Chumvi                                                                  1 ¼ Vijiko vya chai

 
Unga wa ngano                                                    2 Vijiko vya supu

 
Mafuta ya kukaangia

 

 
NAMNA YA KUTAYARISHA NA KUPIKA

 

  1. Osha na kuroweka kunde kwenye bakuli la maji ya baridi usiku mpaka asubuhi.

  2. Saga kwenye mashine (food processor)  kisha mimina kwenye bakuli.

  3. Ongeza vitungu, baking soda, masala, maziwa, na chumvi.

  4. Koroga vizuri halafu tia unga kisha uchanganye pamoja.

  5. Fanya vidonge kama nchi moja kisha ukipenda bana katikati ya mikono na kidole katikati ya bajia.

  6. Kaanga kwenye mafuta ya moto mpaka ziive.

  7. Andaa bajia kwenye sahani na chatini uipendayo.

 

falafi zimekuwa kitafunio

falafi zimekuwa kitafunio changu kikuu. Mashallah.