Njia 10 Za Kuukaribisha Vizuri Mwezi Mtukufu Wa Ramadhwaan
Alhidaaya.com
Inatupasa tumshukuru Allaah (Subhaanahu wa Ta'alaa) kwa kutupa umri tukiwa katika Uislamu na Iymaan hadi kutufikisha tena kukaribia Mwezi mtukufu wa Ramadhwaan. Na hii ni fursa nyingine Anayotupa Allaah Ta’aala katika maisha yetu kushuhudia mwezi huu na kupata fadhila zake.
Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'alaa):
يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا كُتِبَ عَلَيْكُمُ الصِّيَامُ كَمَا كُتِبَ عَلَى الَّذِينَ مِن قَبْلِكُمْ لَعَلَّكُمْ تَتَّقُونَ ﴿١٨٣﴾
Enyi walioamini! Mmefaridhishwa Swiyaam kama ilivyofaridhishwa kwa walio kabla yenu mpate kuwa na taqwa.
أَيَّامًا مَّعْدُودَاتٍ ۚ
(Swiyaam ni) Siku za kuhesabika. [Al-Baqarah: 183-184]
Hii ni neema ya Allaah (Subhaanahu wa Ta'alaa) Ambaye Ametujaalia kuwa na miezi iliyo bora kuliko miezi mingine au siku bora au masaa bora kuliko mengine, ambazo thawabu zake za mema yanayotendeka humo huwa ni zaidi ya nyakati nyingine. Mfano wake, (na Allaah Ana Mifano bora kabisa kulikoni ya yote) ni kama kunapokuwa na mauzo yaliyopunguzwa bei dukani (sale), ambayo kawaida yake huwekwa kwa muda mdogo tu maalum. Na muda huu mtu huweza kununua vitu vingi kwa malipo kidogo tu. Basi Ramadhwaan ni mwezi mmoja tu, lakini malipo yake huwa ni mengi kuliko hata malipo ya miezi yote mingine. Ikiwa mtu atatimiza Swawm yake inavyopaswa na kufanya mema mengi, na akawa katika twaa'ah (utiifu) kamili, taqwa na kuomba maghfirah, basi Muislamu hutoka katika mwezi huu akiwa amechuma thawabu tele na ameghufuriwa madhambi yake.
Amesema Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam):