062 - Al-Jumua'ah

 

الْجُمُعَة

 

062-Al-Jumu’ah

 

 062-Al-Jumu’ah: Utangulizi Wa Suwrah

 

Alhidaaya.com

 

 

بِسْمِ اللَّـهِ الرَّحْمَـٰنِ الرَّحِيمِ

 

 

 

يُسَبِّحُ لِلَّـهِ مَا فِي السَّمَاوَاتِ وَمَا فِي الْأَرْضِ الْمَلِكِ الْقُدُّوسِ الْعَزِيزِ الْحَكِيمِ﴿١﴾

1. Vinamsabbih Allaah Pekee vilivyomo katika mbingu na vilivyomo katika ardhi[1], Mfalme, Ametakasika na sifa zote hasi, Mwenye Enzi ya Nguvu Asiyeshindika, Mwenye Hikmah wa yote.

 

 

 

 

هُوَ الَّذِي بَعَثَ فِي الْأُمِّيِّينَ رَسُولًا مِّنْهُمْ يَتْلُو عَلَيْهِمْ آيَاتِهِ وَيُزَكِّيهِمْ وَيُعَلِّمُهُمُ الْكِتَابَ وَالْحِكْمَةَ وَإِن كَانُوا مِن قَبْلُ لَفِي ضَلَالٍ مُّبِينٍ﴿٢﴾

2. Yeye Ndiye Aliyepeleka Rasuli kwa wasiojua kusoma wala kuandika, atokanaye nao wenyewe, anawasomea Aayaat Zake na Anawatakasa, na Anawafunza Kitabu na Hikmah[2], nao (kwa hakika) walikuwa hapo kabla katika upotofu bayana.

 

 

 

 

وَآخَرِينَ مِنْهُمْ لَمَّا يَلْحَقُوا بِهِمْ ۚ وَهُوَ الْعَزِيزُ الْحَكِيمُ﴿٣﴾

3. Na wengineo ambao bado hawajakutana nao. Naye Ndiye Mwenye Enzi ya Nguvu Asiyeshindika, Mwenye Hikmah wa yote.[3]

 

 

 

 

ذَٰلِكَ فَضْلُ اللَّـهِ يُؤْتِيهِ مَن يَشَاءُ ۚ وَاللَّـهُ ذُو الْفَضْلِ الْعَظِيمِ﴿٤﴾

4. Hiyo ni Fadhila ya Allaah Humpa Amtakaye, na Allaah Ni Mwenye fadhila adhimu.

 

 

 

 

مَثَلُ الَّذِينَ حُمِّلُوا التَّوْرَاةَ ثُمَّ لَمْ يَحْمِلُوهَا كَمَثَلِ الْحِمَارِ يَحْمِلُ أَسْفَارًا ۚ بِئْسَ مَثَلُ الْقَوْمِ الَّذِينَ كَذَّبُوا بِآيَاتِ اللَّـهِ ۚ وَاللَّـهُ لَا يَهْدِي الْقَوْمَ الظَّالِمِينَ﴿٥﴾

5. Mfano wa wale waliobebeshwa Tawraat, kisha wasiibebe ni kama mfano wa punda abebaye mijalada ya vitabu. Ubaya ulioje mfano wa watu waliokadhibisha Aayaat (na Ishara, Dalili) za Allaah! Na na Allaah Haongoi watu madhalimu.[4]

 

 

 

 

قُلْ يَا أَيُّهَا الَّذِينَ هَادُوا إِن زَعَمْتُمْ أَنَّكُمْ أَوْلِيَاءُ لِلَّـهِ مِن دُونِ النَّاسِ فَتَمَنَّوُا الْمَوْتَ إِن كُنتُمْ صَادِقِينَ﴿٦﴾

6. Sema: Enyi Mayahudi! Mkidai kuwa nyinyi ni vipenzi vya Allaah pasina watu wengine, basi tamanini mauti, mkiwa ni wasemao kweli.

 

 

 

 

وَلَا يَتَمَنَّوْنَهُ أَبَدًا بِمَا قَدَّمَتْ أَيْدِيهِمْ ۚ وَاللَّـهُ عَلِيمٌ بِالظَّالِمِينَ﴿٧﴾

7. Na wala hawatayatamani abadani kwa sababu ya yale iliyotanguliza mikono yao, na Allaah Anawajua vyema madhalimu.[5]

 

 

 

 

قُلْ إِنَّ الْمَوْتَ الَّذِي تَفِرُّونَ مِنْهُ فَإِنَّهُ مُلَاقِيكُمْ ۖ ثُمَّ تُرَدُّونَ إِلَىٰ عَالِمِ الْغَيْبِ وَالشَّهَادَةِ فَيُنَبِّئُكُم بِمَا كُنتُمْ تَعْمَلُونَ﴿٨﴾

8. Sema: Hakika hayo mauti mnayoyakimbia, hakika yatakukuteni tu! Kisha mtarudishwa kwa Mjuzi wa ghaibu na dhahiri. Atakujulisheni yale mliyokuwa mkiyatenda.

 

 

 

 

يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا إِذَا نُودِيَ لِلصَّلَاةِ مِن يَوْمِ الْجُمُعَةِ فَاسْعَوْا إِلَىٰ ذِكْرِ اللَّـهِ وَذَرُوا الْبَيْعَ ۚ ذَٰلِكُمْ خَيْرٌ لَّكُمْ إِن كُنتُمْ تَعْلَمُونَ﴿٩﴾

9. Enyi walioamini! Inaponadiwa kwa ajili ya Swalaah siku ya Ijumaa, basi kimbilieni kwenda kumdhukuru Allaah na acheni kuuza na kununua. Hivyo ni kheri kwenu zaidi mkiwa mnajua.[6]

 

 

 

 

فَإِذَا قُضِيَتِ الصَّلَاةُ فَانتَشِرُوا فِي الْأَرْضِ وَابْتَغُوا مِن فَضْلِ اللَّـهِ وَاذْكُرُوا اللَّـهَ كَثِيرًا لَّعَلَّكُمْ تُفْلِحُونَ﴿١٠﴾

10. Na inapomalizika Swalaah, basi tawanyikeni katika ardhi, na tafuteni Fadhila za Allaah, na mdhukuruni Allaah kwa wingi[7] ili mpate kufaulu.

 

 

 

 

وَإِذَا رَأَوْا تِجَارَةً أَوْ لَهْوًا انفَضُّوا إِلَيْهَا وَتَرَكُوكَ قَائِمًا ۚ قُلْ مَا عِندَ اللَّـهِ خَيْرٌ مِّنَ اللَّـهْوِ وَمِنَ التِّجَارَةِ ۚ وَاللَّـهُ خَيْرُ الرَّازِقِينَ﴿١١﴾

11. Na wanapoona tijara au pumbao wanaikimbilia na wanakuacha umesimama. Sema: Yaliyoko kwa Allaah ni bora zaidi kuliko pumbao na tijara, na Allaah Ni Mbora wa wenye kuruzuku.[8]

 

 

 

[1] Kila Kitu Kinamsabbih Allaah (عزّ وجلّ):

 

Rejea Al-Hashr (57:1) kwenye rejea zinazotaja viumbe na vitu Alivyoviumba Allaah kuwa vinamsabbih Yeye Allaah (عزّ وجلّ).

 

[2]  Fadhila Za Waumini Kutumiwa Nabiy Muhammad (صلى الله عليه وآله وسلم):

 

Anasema pia Allaah (سبحانه وتعالى) Kauli Yake kama hii katika Al-Baqarah (2:151), Aal-‘Imraan (3:164). Na duaa ya Nabiy Ibraahiym (عليه السّلام) alipoomba:

 

رَبَّنَا وَابْعَثْ فِيهِمْ رَسُولًا مِّنْهُمْ يَتْلُو عَلَيْهِمْ آيَاتِكَ وَيُعَلِّمُهُمُ الْكِتَابَ وَالْحِكْمَةَ وَيُزَكِّيهِمْ ۚ إِنَّكَ أَنتَ الْعَزِيزُ الْحَكِيمُ ﴿١٢٩﴾

“Rabb wetu, Wapelekee Rasuli miongoni mwao atakayewasomea Aayaat Zako na atakayewafunza Kitabu na Hikmah na atakayewatakasa. Hakika Wewe Ni Mwenye Enzi ya Nguvu Asiyeshindika, Mwenye Hikmah wa yote.” [Al-Baqarah (2:129)]

 

[3] Sababun-Nuzuwl (Sababu Ya Kuteremshwa) Aayah Au Suwrah:

 

Bonyeza kiungo kifuatacho:  

 

062-Asbaabun-Nuzuwl: Al Jumu'ah Aayah 06: وَآخَرِينَ مِنْهُمْ لَمَّا يَلْحَقُوا بِهِمْ

 

Kauli Yake Allaah (سبحانه وتعالى):

 

حَدَّثَنِي عَبْدُ الْعَزِيزِ بْنُ عَبْدِ اللَّهِ، قَالَ حَدَّثَنِي سُلَيْمَانُ بْنُ بِلاَلٍ، عَنْ ثَوْرٍ، عَنْ أَبِي الْغَيْثِ، عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ، رضى الله عنه قَالَ كُنَّا جُلُوسًا عِنْدَ النَّبِيِّ صلى الله عليه وسلم فَأُنْزِلَتْ عَلَيْهِ سُورَةُ الْجُمُعَةِ ‏ وَآخَرِينَ مِنْهُمْ لَمَّا يَلْحَقُوا بِهِمْ قَالَ قُلْتُ مَنْ هُمْ يَا رَسُولَ اللَّهِ فَلَمْ يُرَاجِعْهُ حَتَّى سَأَلَ ثَلاَثًا، وَفِينَا سَلْمَانُ الْفَارِسِيُّ، وَضَعَ رَسُولُ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم يَدَهُ عَلَى سَلْمَانَ ثُمَّ قَالَ ‏"‏ لَوْ كَانَ الإِيمَانُ عِنْدَ الثُّرَيَّا لَنَالَهُ رِجَالٌ ـ أَوْ رَجُلٌ ـ مِنْ هَؤُلاَءِ ‏"‏‏.‏

Amesimulia Abul-Ghayth (رضي الله عنه) kutoka kwa Abuu Hurayrah (رضي الله عنه): Tulikuwa tumeketi pamoja na Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) akateremshiwa Suwrah Al-Jumu’ah:

وَآخَرِينَ مِنْهُمْ لَمَّا يَلْحَقُوا بِهِمْ ۚ وَهُوَ الْعَزِيزُ الْحَكِيمُ﴿٣﴾

“Na wengineo ambao bado hawajakutana nao. Naye Ndiye Mwenye Enzi ya Nguvu Asiyeshindika, Mwenye Hikmah wa yote.” [Al-Jumu’a (62:3)]

 

Nikauliza: Ni akina nani hao Ee Rasuli wa Allaah? Hakunijibu mpaka nilipomuuliza mara ya tatu. Na kati yetu alikuwapo Salmaan Al-Faarisiyy (رضي الله عنه). Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) akaweka mkono wake juu ya Salmaan, kisha akasema: “Lau kama imaan ingalikuwa kwenye ath-thurayyaa (mojawapo wa sayari) wangaliifikia watu (au) mtu katika watu hawa (yaani jamaa za akina Salmaan Al-Faarisiyy).” [Al-Bukhaariy Kitabu Cha Tafsiyr (65)]

 

[4] Mfano Wa Punda Abebaye Mijalada Ya Vitabu:

 

مَثَلُ الَّذِينَ حُمِّلُوا التَّوْرَاةَ ثُمَّ لَمْ يَحْمِلُوهَا كَمَثَلِ الْحِمَارِ يَحْمِلُ أَسْفَارًا ۚ

“Mfano wa wale waliobebeshwa Tawraat, kisha wasiibebe ni kama mfano wa punda abebaye mijalada ya vitabu.”

 

Mtu kama huyo anafanana na punda (mnyama wa kubeba mizigo), kwa vile hapati faida yoyote kwa kule kubeba vitabu vingi mgongoni kwake. Halikadhalika mtu huyo hapati faida yoyote kwa kuswali Swalaah ya Ijumaa. Na hii ni kutokana na katazo la kuzungumza katika Swalaah ya Ijumaa kama ilivyotajwa katika Hadiyth ifuatayo:

 

عَنِ ابْنِ عَبَّاسٍ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم   مَنْ تَكَلَّمَ يَوْمَ اَلْجُمُعَةِ وَالْإِمَامُ يَخْطُبُ فَهُوَ كَمَثَلِ اَلْحِمَارِ يَحْمِلُ أَسْفَارًا، وَاَلَّذِي يَقُولُ لَهُ: أَنْصِتْ، لَيْسَتْ لَهُ جُمُعَةٌ   رَوَاهُ أَحْمَدُ، بِإِسْنَادٍ لَا بَأْسَ بِهِ

 وَهُوَ يُفَسِّرُ حَدِيثَ أَبِي هُرَيْرَةَ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُ  فِي "اَلصَّحِيحَيْنِ" مَرْفُوعًا: إِذَا قُلْتَ لِصَاحِبِكَ: أَنْصِتْ يَوْمَ اَلْجُمُعَةِ وَالْإِمَامِ يَخْطُبُ، فَقَدْ لَغَوْتَ 

Amesimulia Ibn ‘Abbaas (رضي الله عنه): Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: “Mwenye kuzungumza siku ya Ijumaa wakati Imaam anakhutubia, basi yeye ni kama punda aliyebeba vitabu. Na anayemuambia: Nyamaza! Basi huyo hana Ijumaa.” [Imetolewa na Ahmad, kwa Isnaad isiyo na ubaya wowote]

 

[5] Hakuna Atakayeweza Kuyakimbia Mauti!

 

Kila nafsi itaonja mauti. Anasema Allaah (سبحانه وتعالى) katika Kauli Zake zifuatazo:

 

كُلُّ نَفْسٍ ذَائِقَةُ الْمَوْتِ ۗ وَإِنَّمَا تُوَفَّوْنَ أُجُورَكُمْ يَوْمَ الْقِيَامَةِ ۖ فَمَن زُحْزِحَ عَنِ النَّارِ وَأُدْخِلَ الْجَنَّةَ فَقَدْ فَازَ ۗ وَمَا الْحَيَاةُ الدُّنْيَا إِلَّا مَتَاعُ الْغُرُورِ ﴿١٨٥﴾

“Kila nafsi itaonja mauti. Na hakika mtalipwa kikamilifu ujira wenu Siku ya Qiyaamah. Basi atakayewekwa mbali na moto na akaingizwa Jannah, huyo kwa yakini amefuzu. Na uhai wa dunia si lolote ila ni starehe ya udanganyifu.” [Aal-‘Imraan (3:185)]

 

كُلُّ نَفْسٍ ذَائِقَةُ الْمَوْتِ ۗ وَنَبْلُوكُم بِالشَّرِّ وَالْخَيْرِ فِتْنَةً ۖ وَإِلَيْنَا تُرْجَعُونَ ﴿٣٥﴾

“Kila nafsi itaonja mauti.  Na Tutakujaribuni kwa mitihani ya shari na kheri. Na Kwetu mtarejeshwa.” [Al-Anbiyaa (21:35)]

 

كُلُّ نَفْسٍ ذَائِقَةُ الْمَوْتِ ۖ ثُمَّ إِلَيْنَا تُرْجَعُونَ ﴿٥٧﴾

“Kila nafsi itaonja mauti, kisha Kwetu mtarejeshwa. [Al-‘Ankabuwt (29:57)]

 

Na akuna atakayeweza kukimbia mauti hata awe katika jengo la imara vipi kama Anavyosema Allaah (سبحانه وتعالى):

أَيْنَمَا تَكُونُوا يُدْرِككُّمُ الْمَوْتُ وَلَوْ كُنتُمْ فِي بُرُوجٍ مُّشَيَّدَةٍ ۗ  

“Popote mtakapokuwa yatakufikieni mauti, japo mkiwa katika minara (au ngome) imara na madhubuti.” [An-Nisaa (4:78)]

 

Na waliokusudiwa katika Aayah hizo za Suwrah hii Al-Jumu’ah (62:6-7) ni Mayahudi, ni sawa kukusudiwa kwao katika Aayah zifuatazo:

 

قُلْ إِن كَانَتْ لَكُمُ الدَّارُ الْآخِرَةُ عِندَ اللَّـهِ خَالِصَةً مِّن دُونِ النَّاسِ فَتَمَنَّوُا الْمَوْتَ إِن كُنتُمْ صَادِقِينَ ﴿٩٤﴾ وَلَن يَتَمَنَّوْهُ أَبَدًا بِمَا قَدَّمَتْ أَيْدِيهِمْ ۗ وَاللَّـهُ عَلِيمٌ بِالظَّالِمِينَ ﴿٩٥﴾

“Sema: Ikiwa nyumba ya Aakhirah iliyoko kwa Allaah ni makhsusi kwenu pekee pasi na watu wengine, basi tamanini mauti mkiwa ni wakweli. Na hawatoyatamani abadani kwa sababu ya iliyoyatanguliza mikono yao. Na Allaah Ni Mjuzi wa madhalimu.” [Al-Baqarah (2:94-95)]

 

[6] Umuhimu Wa Siku Ya Ijumaa Na Swalaah Ya Ijumaa Na Fadhila Zake:

 

Siku ya Ijumaa ni siku adhimu kwa Waislamu na fadhila zake ni tele. Pia mahimizo ya Swalaah ya Ijumaa, pamoja na fadhila zake, na matahadharisho ya kutokuhudhuria Swalaah ya Ijumaa yametajwa katika Hadiyth kadhaa za Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم).

 

Miongoni mwa himizo na fadhila zake ni Hadiyth ifuatayo:

 

حعَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ ـ رضى الله عنه ـ أَنَّ رَسُولَ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم قَالَ ‏ "‏ مَنِ اغْتَسَلَ يَوْمَ الْجُمُعَةِ غُسْلَ الْجَنَابَةِ ثُمَّ رَاحَ فَكَأَنَّمَا قَرَّبَ بَدَنَةً، وَمَنْ رَاحَ فِي السَّاعَةِ الثَّانِيَةِ فَكَأَنَّمَا قَرَّبَ بَقَرَةً، وَمَنْ رَاحَ فِي السَّاعَةِ الثَّالِثَةِ فَكَأَنَّمَا قَرَّبَ كَبْشًا أَقْرَنَ، وَمَنْ رَاحَ فِي السَّاعَةِ الرَّابِعَةِ فَكَأَنَّمَا قَرَّبَ دَجَاجَةً، وَمَنْ رَاحَ فِي السَّاعَةِ الْخَامِسَةِ فَكَأَنَّمَا قَرَّبَ بَيْضَةً، فَإِذَا خَرَجَ الإِمَامُ حَضَرَتِ الْمَلاَئِكَةُ يَسْتَمِعُونَ الذِّكْرَ ‏"‏‏.‏

Amesimulia Abu Hurayrah (رضي الله عنه): Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: “Mtu yeyote anayeoga siku ya Ijumaa kwa mfano wa ghuslu (josho) la janaba, kisha anakwenda kuswali (mnamo saa ya kwanza, yaani mapema), ni mithili ya kuwa katoa dhabihu (swadaqa) ngamia. Na mtu yeyote anayekwenda mnamo saa ya pili ni mithili ya kuwa katoa dhabihu ng’ombe. Na yeyote anayekwenda saa ya tatu, basi ni kama katoa dhabihu kondoo dume mwenye pembe. Na yeyote anayekwenda saa ya nne, basi huyo ni kama katoa dhabihu ya kuku jike. Na yeyote anayekwenda saa ya tano basi huyo ni kama katoa yai. Imaam anapokuja (anapoanza kutoa khutba), Malaika huhudhuria kuisikiliza khutba.” [Al-Bukhaariy Kitabu Cha Ijumaa (11)]

 

Matahadharisho Ya Kutokuhudhuria Swalaah Ya Ijumaa:

 

عَنْ أَبِي الْجَعْدِ الضَّمْرِيِّ، - وَكَانَتْ لَهُ صُحْبَةٌ - أَنَّ رَسُولَ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم قَالَ ‏ "‏ مَنْ تَرَكَ ثَلاَثَ جُمَعٍ تَهَاوُنًا بِهَا طَبَعَ اللَّهُ عَلَى قَلْبِهِ ‏"‏ ‏.  رواه أحمد وأصحاب السنن

Amesimulia Abuu Al-Ja’d Adhw-Dhwamriyy (رضي الله عنه): Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: “Atakayeacha (kuswali Swalaah ya) Ijumaa mara tatu bila ya sababu yoyote, Allaah Humpiga muhuri katika moyo wake.  [Ahmad na wapokezi wa Hadiyth wengine wenye vitabu vya Sunnan]

 

 

عن ابن عمر وأبي هريرة أَنَّهُمَا، سَمِعَا رَسُولَ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم يَقُولُ عَلَى أَعْوَادِ مِنْبَرِهِ ‏ "‏ لَيَنْتَهِيَنَّ أَقْوَامٌ عَنْ وَدْعِهِمُ الْجُمُعَاتِ أَوْ لَيَخْتِمَنَّ اللَّهُ عَلَى قُلُوبِهِمْ ثُمَّ لَيَكُونُنَّ مِنَ الْغَافِلِينَ ‏"‏ ‏

Amesimulia Ibn 'Umar na Abuu Hurayrah (رضي الله عنهما)  kwamba wamemsikia Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم)   akiwa juu ya mimbari yake ya mbao akisema: “Wasiohudhuria  Swalaah ya Ijumaa  wabadilishe  mtindo wao huo, au sivyo Allaah Atawapiga mihuri katika nyoyo zao  na watakuwa  miongoni mwa walioghafilika.” [Muslim]

 

Somo hili la fadhila za Siku ya Ijumaa na Swalaah ya Ijumaa ni pana. Bonyeza viungo vifuatavyo kupata faida zake tele:

11-Swahiyh Al-Bukhaariy: Kitabu Cha Ijumaa - كتاب الجمعة

12-Buluwgh Al-Maraam: Kitabu Cha Swalaah: Mlango Wa Swalaatul-Jumu'ah (Swalaah Ya Ijumaa)

048-Swahiyh Fiqh As-Sunnah: Mlango Wa Swalaah: Swalaah Ya Ijumaa

051-Swahiyh Fiqh As-Sunnah: Mlango Wa Swalaah: Khutbah Ya Ijumaa Na Hukmu Zinazomkhusu Khatibu

 

053-Swahiyh Fiqh As-Sunnah: Mlango Wa Swalaah: Yanayotendwa Katika Swalaah Ya Ijumaa

31-Riyaadhw Asw-Swaalihiyn: Mlango Wa Ubora wa Siku ya Ijumaa na Wajibu wa Kuoga Kwayo na Kujipaka Manukato,Kwenda Mapema,Kuomba Dua Siku ya Ijumaa, Kumswalia Nabiy na Kubainisha Wakati wa Kujibiwa Dua,Kupendeza Kukithirisha Kumtaja Allaah Baada ya Ijumaa

079-Lu-ulu-un-Manthuwrun: Fadhila Za Swalaah Ya Jamaa'ah

082-Lu-ulu-un-Manthuwrun: Fadhila Za Siku Ya Ijumaa Na Kumswalia Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم)

Ibaadah Zipasazo Kutekelezwa Siku Ya Ijumaa

 

[7] Kumdhukuru Allaah (سبحانه وتعالى) Kwa Wingi Jioni Ya Siku Ya Ijumaa:

 

Baada Ya Alasiri na kabla ya Magharibi, kuna fadhila adhimu ya kutakabaliwa mtu duaa yake kutokana na Hadiyth zifuatazo:

 

عَنْ جَابِرِ بْنِ عَبْدِ اللَّهِ (رضي الله عنه) عَنْ رَسُولِ اللَّهِ (صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ) قَالَ: ((يَوْمُ الْجُمُعَةِ اثْنَتَا عَشْرَةَ سَاعَةً ،لاَ يُوجَدُ فِيهَا عَبْدٌ مُسْلِمٌ يَسْأَلُ اللَّهَ شَيْئًا إلاَّ آتَاهُ إِيَّاهُ ، فَالْتَمِسُوهَا آخِرَ سَاعَةٍ بَعْدَ الْعَصْر))

Amesimulia Jaabir bin ‘Abdillaah (رضي الله عنه): Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: “Siku ya Ijumaa kuna masaa kumi na mbili ambayo hapatikani mja Muislamu anayemwomba Allaah kitu ila Anampa, basi itafuteni saa la mwisho baada ya Swalaah ya Alasiri.”  [Swahiyh Abiy Daawuwd (1048), Swahiyh An-Nasaaiy (1388), Swahiyh Al-Jaami’ (8190)]

 

‘Ulamaa wamesema kuhusu saa katika siku ya Ijumaa inayotakabaliwa duaa, kwamba zimetajwa nyakati kadhaa, ila waliyokubaliana zaidi yao ni saa ya mwisho kabla ya Swalaah ya Magharibi.

 

 

Share