107 - Al-Maa’uwn
الْمَاعُون
Al-Maa’uwn: 107
بِسْمِ اللَّـهِ الرَّحْمَـٰنِ الرَّحِيمِ
أَرَأَيْتَ الَّذِي يُكَذِّبُ بِالدِّينِ ﴿١﴾
1. Je, umemuona yule anayekadhibisha malipo?
فَذَٰلِكَ الَّذِي يَدُعُّ الْيَتِيمَ ﴿٢﴾
2. Basi huyo ndiye yule anayemnyanyasa yatima.
وَلَا يَحُضُّ عَلَىٰ طَعَامِ الْمِسْكِينِ ﴿٣﴾
3. Na wala hahamasishi kulisha maskini.
فَوَيْلٌ لِّلْمُصَلِّينَ ﴿٤﴾
4. Basi ole kwa wanaoswali.
الَّذِينَ هُمْ عَن صَلَاتِهِمْ سَاهُونَ ﴿٥﴾
5. Ambao wanapuuza Swalaah zao.
الَّذِينَ هُمْ يُرَاءُونَ ﴿٦﴾
6. Ambao wanajionyesha (riyaa-a).
وَيَمْنَعُونَ الْمَاعُونَ ﴿٧﴾
7. Na wanazuia (pia) misaada ya matumizi madogodogo ya kawaida ya kila siku.
