49-Fadhila Za Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم): Nabiy Pekee Aliyepewa Kauli Za Kusherehi Kitabu Chake

Fadhila Za Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم)

 

49-Nabiy Pekee Aliyepewa Kauli Za Kusherehi Kitabu Chake

 

 

www.alhidaaya.com

 

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

  وَأَنزَلْنَا إِلَيْكَ الذِّكْرَ لِتُبَيِّنَ لِلنَّاسِ مَا نُزِّلَ إِلَيْهِمْ وَلَعَلَّهُمْ يَتَفَكَّرُونَ﴿٤٤﴾

 (Tumewatuma) Kwa hoja bayana na vitabu. Na Tumekuteremshia Ukumbusho (Qur-aan) ili uwabainishie watu yaliyoteremshwa kwao huenda wakapata kutafakari. [An-Nahl: 44]

 

 

Maana yake: “Tumekuteremshia Qur-aan ee Rasuli, ili uwabainishie wazi watu yaliyofichikia katika maana zake, hukmu zake na ili wazingatie (Aayaat) na waongoke kwayo.” [Tafsiyr Al-Muyassar]

 

Hivyo basi anayoyasema katika kusherehi Aayaat za Qur-aan ni Wahyi Aliofunuliwa Na Allaah (سبحانه وتعالى) Ambaye Anasema:

 

 

مَا يَنطِقُ عَنِ الْهَوَىٰ ﴿٣﴾

Na wala hatamki kwa hawaa.

إِنْ هُوَ إِلَّا وَحْيٌ يُوحَىٰ ﴿٤﴾

Hayo si chochote isipokuwa ni Wahy unaofunuliwa. [An-Najm: 3-4]

 

Akasema Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم)  kuthibitisha hayo katika Hadiyth:

 

((أَلَا إِنِّي أُوتِيتُ الْقُرْآنَ وَمِثْلَهُ مَعَهُ)) صحيح رواه أبو داود

((Hakika mimi nimepewa Qur-aan na mfano wake)) [Hadiyth Swahiyh, Abuu Daawuwd]

 

 

 

Share