13-Swahiyh Fiqh As-Sunnah: Mlango Wa Zakaah: Zakaah Ya Mahari

Swahiyh Fiqh As-Sunnah

 

Mlango Wa Zakaah

 

13-Zakaah Ya Mahari

 

Alhidaaya.com

 

 

Mahari ya mwanamke ni mali kama zilivyo mali nyinginezo, na hukmu yake ni hukmu ya mali nyinginezo.

 

1- Kama mwanamke amepokea mahari yake, na ikawa ni katika aina za mali zinazotolewa Zakaah na ikafikia kiwango au kikazidi, basi ataitolea Zakaah ikipitiwa na mwaka.

 

2- Ikiwa mahari ni ya kulipwa siku za mbeleni, basi itakuwa na hukmu ya deni ambayo tumeizungumzia nyuma. Ikiwa mume wake ana uwezo wa kifedha na ni mtu wa kuaminika, basi itambidi mwanamke atoe Zakaah ya mahari yake ambayo iko katika dhima ya mumewe, kwa kuwa matumaini ya kulipwa yapo. Lakini kama ni masikini, basi si lazima mwanamke huyo kutoa Zakaah ya mahari hiyo kwa mujibu wa kauli yenye nguvu. Na anapopokea mahari yake, ataitolea Zakaah ya mwaka mmoja tu.

 

3- Mwanamke akipokea mahari yake, halafu akatalikiwa kabla ya kuingiliwa, kisha mahari ikapitiwa na mwaka na ikafikia kiwango, basi yeye atatoa Zakaah ya nusu ya mahari, na mtalaka wake atatoa nusu nyingine. Allaah Ndiye Mjuzi Zaidi. [Angalia Al-Mughniy (3/52), Jaami’u Ahkaamin Nisaa (2/165) na Kitabu changu cha Fiqhu As-Sunnah Lin Nisaa (uk 217)]

 

 

 

Share