16-Swahiyh Fiqh As-Sunnah: Mlango Wa Hajj Na 'Umrah: Kuingia Makkah

Swahiyh Fiqh As-Sunnah

 

Mlango Wa Hajj Na ‘Umrah

 

16-Kuingia Makkah

 

Alhidaaya.com

 

 

 

 

Sunnah Za Kuingia Makkah

 

1,2,3- Kulala Dhiy Tuwaa, kuoga kwa ajili ya kuingia hapo, na kuingia mchana

 

Ni kwa Hadiyth ya Naafi’u aliyesema: ((Ibn ‘Umar (Radhwiya Allaah ‘anhumaa) alikuwa anapoingia karibu na Al-Haram, huacha Talbiyah, kisha hulala Dhiy Tuwaa, halafu huswali huko Asubuhi na huoga. Na hueleza kuwa Nabiy (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) alikuwa anafanya hivyo)). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Al-Bukhaariy (1573) na Muslim (1259)]

 

 

4- Kuingia Makkah kutokea njia ya juu ya mlimani [Ath-Thaniyyat Al-‘Ulyaa]

 

Ni kwa Hadiyth ya Ibn ‘Umar aliyesema: ((Rasuli wa Allaah (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) alikuwa anaingia kutokea Ath-Thaniyyat Al-‘Ulyaa, na hutokea Ath-Thaniyyat As-Suflaa [Sehemu ya chini ya Makkah])). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Al-Bukhaariy (1575) na Muslim (1257)]

 

5- Kutanguliza mguu wa kulia wakati wa kuingia Al-Masjid Al-Haraam na kuomba kwa kusema:

"يسم الله، اللهم صل على محمد وسلم، اللهم افنح لي أبواب رحمتك"

“Bismil Laah. Ee Allaah! Mpe Rahmah na Amani Muhammad. Ee Allaah! Nifungulie milango ya Rahmah Zako”.

 

[Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Muslim (713), At-Tirmidhiy (314), na An-Nasaaiy (729) bila kumswalia Nabiy. Ipo kwa Abu Daawuwd (465)]

 

 

6- Kunyanyua mikono na kuomba du’aa wakati mtu anapoiona Al-Ka’abah

 

Limethibiti hili toka kwa Ibn ‘Abbaas. [Isnaad yake ni Swahiyh. Imekharijiwa na Ibn Abiy Shaybah (3/96). Angalia Manaasikul Hajj cha Al-Albaaniy (20)]

 

Kisha ataomba du’aa nyepesi. Na akisema:

"اللهم أنت السلام، ومنك السلام، فحينا ربنا بالسلام"

“Ee Allaah! Wewe ni As Salaam (Amani), na Amani inatoka Kwako, basi tuhuishe ee Mola wetu kwa Amani”.

 

..basi ni vyema zaidi kwa vile imethibiti toka kwa Ibn ‘Umar. [Isnaad yake ni Hasan. Imekharijiwa na Al-Bayhaqiy (5/72). Angalia Manaasikul Hajj (20)]

 

7- Atufu Twawaaf ya Kuwasili (Twawaaful Quduwm)

 

Itakuja kuelezewa mbeleni.

 

 

 

Share