25-Hadiyth Al-Qudsiy: Watu Watatu Watakaokuwa Wagomvi Wa Allaah Siku Ya Qiyaamah

Hadiyth Al-Qudsiy

Hadiyth Ya 25

Watu Watatu Watakaokuwa Wagomvi Wa Allaah Siku Ya Qiyaamah

 

عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رَضِيَ اللَّهُ عَنْهُ عَنْ النَّبِيِّ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ قَالَ:  ((قَالَ اللَّهُ ثَلَاثَةٌ أَنَا خَصْمُهُمْ يَوْمَ الْقِيَامَةِ، رَجُلٌ أَعْطَى بِي ثُمَّ غَدَرَ، وَرَجُلٌ بَاعَ حُرًّا فَأَكَلَ ثَمَنَهُ،  وَرَجُلٌ اسْتَأْجَرَ أَجِيرًا فَاسْتَوْفَى مِنْهُ وَلَمْ يُعْطِ أَجْرَهُ)) البخاري, أحمد وابن ماجه

Abu Hurayrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) amehadithia kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: ((Allaah Amesema: Kuna watu watatu watakaokuwa wagomvi Wangu Siku ya Qiyaamah; Mtu aliyetoa neno lake (ahadi) kwa Jina Langu na asitekeleze, mtu aliyemuuza mtu huru na pesa akazitumia; na mtu aliyeajiri mfanyakazi wakakubaliana kisha asimpe ujira wake”. [Al-Bukhaariy, Ahmad na Ibn Maajah]

 

 

Share