001-Unawezaje Kuupata Moyo Wa Mumeo Na Kumridhisha Mola Wako: Utangulii

 

UTANGULIZI

 

Kila jinsi ya sifa njema anastahiki Allaah ambaye Ametufanyia ndoa kuwa ni katika shari’ah ya Dini hii, Akajaalia baina ya wanandoa mapenzi na huruma na Akayafanya hayo kuwa ni dalili na ishara kwa watu wenye kufikiri, Kisha swala na salamu kwa mbora wa viumbe na mpendwa wa kweli Mtume Muhammad (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) mbora wa waume, baba bora na aali na sahaba zake wote.

 

Baada ya hayo:

Famiilia ni tofali la jamii, likitengemaa na jamii hutengamaa kwake kutatimia, familia inaweza kukumbwa na matatizo yatakayotikisa nguzo zake, kuharibu mustakabali wake na kuzuia hilo kabla ya kutuka kwake ni bora kuliko kutibu, ndio maana tukaja na kijitabu hiki kwa mwanamke aliyeolewa kwani yeye ndiye mwenye athari kubwa katika kuitengeneza au kuiharibu familia, hadi pale atakapoweka mguu wake na kusimama katika njia ya furaha ya kweli ili aweze kujibu swali ambalo mara nyingi linapita katika akili za wanawake wengi walioolewa; ‘Je, Ni vipi utauteka moyo wa mume wako na kumridhisha Mola wako?

 

Tunamuomba Allaah Mkarimu Anufaishe kwa kitabu hiki kila msomaji, na Atuonyeshe haki na Atuongoze kwenye haki hiyo, atusamehe makosa yetu na kwa hakika yeye ni muweza wa hilo.

 

Tunamuomba Allaah kwa majina Yake matukufu Atusamehe madhambi yetu na makosa yetu, na Atujaalie sisi kuwa funguo za kheri na kufuli za shari na Aturuzuku ukweli wa maneno na matendo.

 

“…Mola wangu Mlezi! Niwezeshe nishukuru neema Zako ulizonineemesha mimi na wazazi wangu, na nitende mema unayo yapenda. Na unitengenezee dhuriya zangu. Hakika mimi nimetubu kwako, na mimi ni miongoni mwa Waislamu.” (46:15)

 

 

‘Aadil Fat-hi ‘Abdullaah

 

Share