013-Hakimu Wa Kiislamu: Sura Ya Saba

 

SURA YA SABA

 

WAFANYAKAZI WA MAHKAMA

 

 

Wanachuoni wanakubaliana kwamba ni lazima akuwepo karani anayeweza kuandika na awe ndani ya sehemu ya jamii ili kusaidia kazi ya kutoa hati za wito. Awe ni mtu mwenye kuisimamisha na kuifuata Shari’ah na amri zake kuhusiana na vikaza hukumu. Bila ya kusahau, ni lazima karani awe ni mtu anayeaminika na mwenye elimu nzuri ya Fiqhi na akae sehemu ambayo Hakimu atamuona nini anachoandika.

 

Kwa mujibu wa Sheria ya Mahkama, Jaji Mkuu anaweza kuteua watu kwa idadi yoyote kuwa ni wasajili, makarani, wadhamini, wafasiri na maofisa wengine wanaohitajika na Mahkama yoyote. Msajili wa Mahkama Kuu anaweza kuwataka wateuliwa hao kula kiapo.[1]

 





[1] Sheria ya Mahkama, S. 25 na 26.

Share