10-Wasiya Wa Mwisho Wa Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم): Kuna Wakati Waislamu Hutofautiana Juu ya Mambo mengi, Msimamo Wetu Kuhusu Bid’ah Uwe Upi?

 

Kuna Wakati Waislamu Hutofautiana Juu ya Mambo mengi, Msimamo Wetu Kuhusu Bid’ah Uwe Upi?

 

Wanachuoni wengi wa bandia, na wale wa namna yao wanasema, “Acheni jambo hili kwani wakati wake bado. “Kwa hakika, wengi wao wanasema, “Mazungumzo kuhusu bid’ah yanawagawa Waislamu.”

 

Hata hivyo Mjumbe wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alitufundisha tofauti, kama tutafikwa na mtafaruku na kugawanyika, lazima tuepukana na bid’ah. Yeye (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alisema, “Kwa hakika yule atakayeishi (baada yangu) ataona mfarakano mkubwa….”

 

Mpaka Yeye (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) aliposema,

“Na kuweni macho na mambo mapya yaliyozuliwa.”

Tunapozingatia tofauti kubwa kati ya yaliyosemwa na kundi tulilolitaja hapo juu kuhusu suala hili na anachosema Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) tunatakiwa tukumbuke kuwa si rukhsa kufanya ijtihaad (kuweka mbele maoni yake mtu) wakati (ambapo) ijtihaad hiyo inapingana na Aayah iliyo wazi ya Qur-aan au Hadiyth ya Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam).

 

Tusisahau ya kuwa, amri ya Mtume kuhusu bid’ah, inatokana na maamrisho muhimu aliyoyatoa kwa Ummah wake.

 

Baada ya hapo tukumbuke kuwa bid’ah zina sura na rangi nyingi –kuna bid’ah katika imani (‘Aqiydah), katika tawhiyd, katika ibada na katika mu’amalah. Ni bid’ah ipi tutakayoifumbia macho bid’ah katika imani? Itawezekanaje wakati tunajua kuwa usafi katika imani ni wa umuhimu wa juu na ipewe kipaumbele juu ya masuala yote.

 

Tuliwapiga makafiri na mapagani (washirikina) kwa sababu na utupu  na upotofu wa imani zao. Haya basi, vipi bid’ah katika ibada? Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) aliondosha shaka yoyote kuhusu aina hii na kuhusu aina zote za bid’ah aliposema,

“Na kila bid’ah ni upotevu!”

 

Na kamwe hatuwezi kuunganisha Ummah kutokana na upotevu, kwani Mjumbe wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alisema,

 

“Kwa hakika, Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala) Aliukinga Ummah wangu kutokana kuunganika pamoja katika upotevu.”[1]

 

Watu wasipofuata maamrisho ya Allaah, wanajitakia ghadhabu ya Allaah. Fikiria askari anayemuasi afisa mwandamizi wake ambaye si tu ana uwezo, lakini anachukia uasi vile vile, afisa yule atamuadhibu mnyonge wake. Sasa fikiria sisi kumuasi Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala) na kisha kutamani kutoka Kwake Neema, Rehema na Msaada!

 

Haiyumkiniki kimaadili wala kimatendo kwetu sisi kuruhusu kuenea kwa bid’ah na kupenya katika jamii na wakati huo huo kutaraji umoja miongoni mwa Waislamu na nguvu katika Ummah wetu.

Allaah Anasema:

…Hakika Allaah habadili yaliyoko kwa watu mpaka wabadili wao yaliyomo nafsini mwao... (13: 11).

 

Kama tulivyokwishajadili; kule kuwepo tu kwa bid’ah kunasababisha kutoweka kwa Sunan (wingi wa Sunnah). Kukosekana kwa Sunan za Mtume, na kuwepo kwa bid’ah, kuna mtu mwenye akili timamu anayetarajia Waislamu kuungana!

 

 

Kila Bid’ah ni Upotevu

 

Mjumbe wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) anafafanua kuwa mambo mapya yaliyoanzishwa ni uzushi (bid’ah) na njia ya upotevu.

Kwa kuacha Sunnah, tunawaiga Wana wa Israaiyl, ambao waliangamizwa walipojishughulisha na visa, wakitelekeza kutimiza dini yao. Inatajwa kwenye Hadiyth”

 

“Kwa hakika, Wana Israaiyl waliangamizwa, walipojishughulisha na kusimulia visa.”[2]



[1] Hasan, katika silsilah zake mbali mbali; ilisimuliwa na Abu ‘Aaswim katika As-Sunnah katika mlolongo wa nambari, 82, 83 na 84 (nakala ina maoni ya Shaykh wetu -Allaah Awe radhi naye) katika At-Tirmidhiy, na katika vyanzo vingine. Rejea Asw-Swahiyhah (1331) za Adh-Dhwa’iyfah, katika maelezo ya Hadiyth Na.1510.

[2] Ilisimuliwa na At-Twabaraaniy, katika Al-Mu’jam Al-Kabiyr; Abu Nu’aym katika Al-Hilyah; na wengineo. Aidha imetajwa ndani ya As-Swahiyhah (1681). Katika Nihaayah imetajwa, “Ikiwa na maana, waliamini khutbah na kuacha matendo, na hiyo ilikuwa sababu ya kuangamizwa kwao, au kinyume chake: walipoangamizwa kwa sababu ya kuacha matendo, wakajishughulisha na visa.”

Shaykh wetu (Allaah Amuwie radhi) alisema, “Inakubalika kusema ya kuwa sababu ya kuangamizwa kwao ni kuzipa umuhimu watoa khutbah na visa vyao, badala ya kuzingatia Fiqh na elimu yenye manufaa, elimu ambayo ingewasaidia kujua dini yao…Hilo lilipojiri waliangamizwa, mashaka yanayowapata wahubiri leo, na maonyo yao mengi yanatokana na masimulizi ya Wana wa Israaiyl au kutoka kwa Masufi na tunamwomba Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala) Atulinde.”

 

Share